Biblia

MWANAMUME mmoja anayefahamika kama mchungaji katika kanisa moja ameripotiwa kumuua bintiye mwenye umri wa miaka 16 anayeigua ugonjwa wa Down Synbdrome aimtuhumu kama mchawi.

Tukio hili la kushtua lilifichuliwa katika chapisho lililosambaa kwenye jukwaa maarufu la mtandao wa kijamii, X, lililojulikana kama Twitter.

Ndugu mdogo wa msichana huyo alisema baba yao alikusanya familia na kutangaza kifo chake baada ya tukio hilo.

Ndugu mdogo alikumbuka kufungua mlango kumsaidia Dadake kutupa kinyesi chake wakati baba yao alipoingilia kati, akisisitiza ashughulikie mwenyewe. Alitii lakini akaanguka huku akirudi chumbani kwake.

Kijana alisema alimjulisha baba yao, ambaye aliingia chumbani na kuwaambia wengine waondoke wakati yeye akimuhudumia bintiye. Baada ya muda mrefu, Pasta aliwaita watoto wake ndani na kutangaza kufariki kwa binti huyo.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Aliyeshiriki chapisho hilo aliyetambulika kwa jina la @EduEle5 kupitia ukurasa wa X, alifichua kuwa polisi wamepewa taarifa na mchungaji huyo kwa sasa yuko mbioni.

Mamlaka imeanzisha msako na pia inaomba umma usaidizi wa kumpata na kumkamata.

Chapisho hilo lilisomeka, “Mtume Ubong Bassey Etim alimuua bintiye mwenye umri wa miaka 16 huko Calabar baada ya kumshutumu kuwa mchawi ambaye angeweza kubadilika na kuwa nyoka. Msichana huyo mchanga, ambaye alikuwa na ugonjwa wa Down, aliuawa kikatili mnamo Februari 15, 2025, huko Calabar, Jimbo la Cross River.”

“Mke wa mshukiwa aliyeachana naye alifichua kwamba pasta alikuwa na historia ya unyanyasaji wa nyumbani, ambayo ilimlazimu kutoroka nyumbani kwao. Pamoja na hayo, aliendelea kupigania usalama wa watoto wake. Sasa anatoa wito kwa kusaidia kuhakikisha bintiye anapata haki.”

Tazama chapisho hilo hapa;