Jogoo

MAHAKAMA imempata na hatia ya uchafuzi wa mazingira kwa kelele, mfugaji mmoja wa kuku ambaye majirani walirekodi jogoo wake akiwika mara 76 chini ya saa moja.

Mmiliki huyo wa jogoo mkorofi aliagizwa kulipa faini ya zaidi ya pauni 3,000 (Shilingi 490, 247) baada ya majirani kulalamika kuhusu kuwika kwake bila kukoma.

Kesi hiyo ya ajabu iliripotiwa Kaskazini Mashariki ya Derbyshire nchini Uingereza ambapo maafisa wa halimashauri walitumia vifaa vya uchunguzi wa kitaalamu na kupata ndege huyo anayesumbua akiwika karibu mara 80 katika muda wa chini ya saa moja.

Mmiliki wake, Derek Bower, awali alipewa notisi ya kuachwa lakini baadaye aliitwa kufika mbele ya mahakimu wa Derby.

Halmashauri ya Wilaya ya Kaskazini Mashariki ya Derbyshire, ambayo iliweka kesi hiyo hadharani wiki hii kufuatia kusikilizwa mnamo Desemba, inasema Huduma yake ya Afya ya Mazingira ilipokea malalamiko ya kelele kuhusu jogoo kuwika katika Upande wa Kaskazini, New Tupton, BBC Derbyshire iliripoti.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Uchunguzi ulisababisha vifaa maalum vya kufuatilia kelele kufungwa na Afisa wa Afya ya Mazingira ili kurekodi mzunguko na kiwango cha kelele kutoka kwa makazi ya mfugaji huyo wa kuku.

Ilionyesha mara kwa mara kuwika ni "kupindukia", na jogoo akiwika siku nzima, ambayo iliathiri kwa kiasi kikubwa majirani.

Kisha afisa wa Afya ya Mazingira alifanya ukaguzi kwenye makazi na kurekodi ndege huyo mkorofi akiwika mara 76 kati ya saa 05:53 na 06:43.

Baraza hilo lilisema lilitoa notisi kwa Bw Bower, lakini hakushirikiana na mamlaka hivyo kesi hiyo ilipelekwa katika mahakama ya jiji.

Bw Bower alishindwa kuhudhuria kesi hiyo tarehe 9 Desemba 2024 na alitozwa faini ya £660 bila kuwepo kwake.

Pia aliagizwa kulipa ada ya ziada ya £924 (Sh150,996) na £1,623.96 (Sh265,380) kwa gharama, kulipwa ndani ya siku 28.