
MWANAHABARI nguli wa taarifa za spoti mitandaoni, Fabrizio Romano ameonyesha furaha ya kipekee baada ya gwiji wa soka Lionel Messi kutoa maoni kwenye chapisho lake.
Muitaliano huyo anayefurahia ufuasi wa zaidi ya watu milioni 22 kwenye Facebook alichapisha taarifa kuhusu kinywaji kipya anachokitumia mwanasoka Lionel Messi na wanatimu wenzake Inter Miami.
“Mas+ ya Lionel Messi sasa ndicho kinywaji rasmi cha kuongeza maji mwilini cha Inter Miami,” Fabrizio Romano alichapisha akifuatisha na picha ya Messi akinywa kinywaji hicho uwanjani.
Katika hali nadra zaidi kushuhudiwa, Messi mwenye ufuasi wa zaidi ya watu milioni 117 alifika kwenye chapisho hilo na kutoa maoni yake kwa kutumia emoji za kuinua mikono juu.
Romano ambaye hakuwa anaamini kabisa alipiga screenshot hiyo na kumshukuru Messi kwa kugundua kwamba anamfuatilia mitandaoni na pia kushukuru wafuasi wake kwa kufanya ukurasa wake kuwavutia watu maarufu.
“Najivunia ukurasa wangu wa Facebook na jumuiya. Kuona Leo Messi akija hapa, kusoma chapisho letu na kutoa maoni… ni wakati mwafaka kwangu,” Romano aliandika.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!