2baba atambuisha mpenzi mpya wiki mbili baada ya ndoa ya miaka 13 kuvunjika

WIKI mbili tu baada ya msanii mkwasi kutoka Nigeria, 2Baba Idibia kutangaza kuvunjika kwa ndoa yake ya miaka 13 na Annie Macaulay, ripoti zimeibuka kwamba sasa anatarajia mtoto na mpenzi mpya.

Uvumi wa Idibia kuwa katika mahusiano na Mrembo mwanasiasa kwa jina Natasha Osawaru, msanii huyo mwenyewe alithibithisha tetesi hizo mapema Jumanne katika video kupitia Instagram.

"Ndio, nimeona mambo mengi sana, simulizi nyingi za uongo na upuuzi mbaya baada ya kupost vitu hivyo. Mh. Natasha ameburuzwa, anaitwa kila aina ya majina, na kupachikwa jina la mvunja nyumba. Lakini ni mwanamke mdogo, mwenye kipaji, wa kushangaza na hakuwa na uhusiano wowote na kilichotokea kati yangu na Annie," 2Baba alisema kwa uthabiti.

Na kama uvumi huo hautoshi, hitmaker huyo wa ‘African Queen’ na mpenzi wake mpya sasa wameripotiwa kuwa wamo mbioni kuitwa wazazi, ikiwa haijapita hata mwezi kabla ya kuachana na Anne.

Ripoti hiyo ilishirikiwa na mwanablogu mpelelezi na mwanahabari, Stella Dimoko-Korkus, katika chapisho la Instagram.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Kulingana na Stella Dimoko-Korkus, 2Baba na Natasha wanapendana na wanakaribia kufunga ndoa, huku washirika wa karibu wakifichua kuwa wanatarajia mtoto wao wa kwanza.

Chapisho hilo linasema, "2face idibia, mwimbaji ambaye huwezi kuacha kumzungumzia (kwa sasa) na Mheshimiwa Natasha Igbinedo wa familia maarufu ya Igbinedo ya ufalme wa Benin wako katika mapenzi na wanakaribia kuanzisha familia."

"Wana mimba ya mtoto wao wa kwanza na mwimbaji huyo alikiri kwenye video mapema Jumanne Februari 12, 2/25 asubuhi kwamba anampenda na anataka kumuoa".

2baba na mpenzi mpya watarajia mtoto

Mwimbaji na mke wa sasa walioachana, Annie, ambao walifunga pingu za maisha mnamo 2012, walikuwa wameonekana kwa muda mrefu kama moja ya wanandoa mashuhuri wa kudumu wa Nigeria.

Harusi yao ya kifahari huko Dubai mnamo 2013 ilikuwa ya kupendeza, na hadithi yao ya mapenzi haikufa katika wimbo wake wa African Queen, ambapo Annie alicheza mapenzi yake.

Walakini, nyufa katika ndoa yao zilikuwa zimeonekana kwa miaka. Uhusiano wao ulikuwa na kashfa za kudanganya, mabishano ya umma na mapambano ya kibinafsi, lakini matokeo ya mwisho hayakujulikana.