JIMBO moja la kanisa Katoliki nchini Nigeria limemsimamisha kazi kasisi wao baada ya kugundua kwamba ako na ndoa ya kisiri nchini Marekani.
Padre Daniel Okanatotor Oghenerukevwe aliripotiwa kuvuliwa ukasisi baada ya madai hayo kuthibitishwa na jimbo lake huko Delta.
Katika taarifa iliyopewa jina la "Amri ya Kusimamishwa" ya Alhamisi, Januari 16, 2025, na iliyotolewa kwa waandishi wa habari Jumapili, Dayosisi hiyo ilithibitisha kwamba padre alifunga ndoa na Bi harusi mnamo Desemba 29, 2024, katika Kanisa la Streams of Joy huko Dallas, Marekani.
Barua hiyo ya kusimamishwa, iliyosainiwa na Rt. Kasisi Anthony Ovayero Ewherido, Askofu wa Warri, na Fr. Clement Abobo, Chansela/Mthibitishaji, alinukuu Canon 1394 S1, ambayo inaweka adhabu ya kusimamishwa kazi kwa makasisi wanaojaribu kuoa.
Taarifa hiyo ilisomeka kwa sehemu:
“Kwa hatua hii, Mchungaji Fr. Daniel Okanatotor Oghenerukevwe amesababisha kusimamishwa kazi kwa sententiae, na mimi, Kasisi Anthony Ovayero Ewherido, ninaamuru rasmi kwamba asimamishwe kutoka kwa huduma takatifu.”
Dayosisi hiyo ilifichua kwamba padre huyo aliomba kuachiliwa kutoka kwa majukumu yake ya kisheria mnamo Novemba 30, 2024.
Hata hivyo, licha ya kutakiwa kutoa nyaraka muhimu za kurasimisha mchakato huo, Fr. Oghenerukevwe aliendelea na ndoa bila kukamilisha utaratibu.
Kwa sababu hiyo, haruhusiwi kujionyesha kama padre wa Jimbo la Warri, na athari zote za kisheria za kusimamishwa kazi zinaonekana mara moja (taz. Can. 1333).
Dayosisi hiyo pia ilisema kuwa Fr. Oghenerukevwe anabaki na haki ya kukata rufaa ya kusimamishwa kazi na kutaka kubatilishwa au kufanyiwa marekebisho amri hiyo ikiwa ataonyesha nia ya kufanya mageuzi.
Taarifa hiyo ilihitimisha:
"Mungu amjalie neema ya kutafakari juu ya hali hii na kumuongoza kwenye njia ya upatanisho."
Picha za ndoa hiyo, ambayo inasemekana kusambazwa sana kwenye mitandao ya kijamii, inaaminika kuwa ndiyo iliyochochea majibu ya haraka ya dayosisi hiyo.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!