SHULE ya Upili ya Bahari Girls imekuwa shule ya kwanza kabisa ya upili katika Kaunti ya Kilifi kutoa mwanafunzi wa kike aliyepata alama ya wastani ya ‘A’ katika Cheti cha Elimu ya Sekondari ya Kenya (KCSE).


Grace Sidi Karisa, mwanafunzi wa shule ya wasichana karibu na mji wa Kilifi, alipata alama ya wastani ya A katika matokeo ya mtihani wa KCSE yaliyotoka hivi punde, na kuwa msichana wa kwanza kusoma katika shule moja katika kaunti hiyo kupata daraja hilo.


Siku ya Ijumaa, wazazi, wanafunzi wenzake, na majirani walisherehekea ufanisi wa Sidi nyumbani kwake eneo la Matsangoni kaunti ndogo ya Kilifi Kaskazini, ambapo walimbeba bega juu huku wakimpongeza kwa kazi hiyo kubwa.


Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Wazazi wake na mkuu wa shule hiyo, Silvano Hamaro, walisema wamefurahishwa na mafanikio hayo makubwa licha ya kwamba Sidi anatoka katika maisha duni.


Wakati huo huo, walimu na wanafunzi katika Chuo cha Istqama katika kaunti ndogo ya Malindi, walivunja wimbo na dansi baada ya kuibuka kuwa shule bora zaidi ndani ya kaunti hiyo ndogo, na alama za wastani za 'B-' (B-minus).


Akizungumza na waandishi wa habari nyumbani kwa wazazi wake, Grace alisema anatamani kusomea udaktari na kuwa daktari.


Mkuu wa shule hiyo, Maalim Goso Mohamed, alisema shule hiyo ilirekodi wanafunzi watatu waliopata alama ya wastani ya B+ licha ya wanafunzi hao kutoka katika mazingira duni na kutegemea mpango wa ufadhili wa shule.


 


Alisema kati ya watahiniwa 47 shule iliyofanya mitihani hiyo, wanafunzi 37, sawa na asilimia 79 walipata daraja la wastani la C+ na waliohitimu kujiunga na chuo kikuu moja kwa moja.


 


Mohamed alisema uongozi wa shule unafadhili wanafunzi wanaoishi katika mazingira magumu kwa kuwaruhusu kulipa nusu ya ada inayotakiwa hivyo kuwapunguzia mzigo familia zao hivyo kuwapa utulivu wa moyo wanafunzi hao wanaposoma.