December 11, 2024
1 min read

Mwanafunzi wa chuo kikuu cha
Zetech mwenye umri wa miaka 21 amepatikana amefariki baada ya kisa
kinachoshukiwa kuwa cha kujitoa uhai katika ghorofa aliyokuwa akiishi katika
eneo la Thika, Kiambu.
Mwili wa Ryan Kitari ulipatikana
siku ya Jumatano asubuhi ukining'inia kwenye ukuta wa ghorofa ya juu ya jumba
alimokuwa akiishi.
Aliacha barua ya kujitoa uhai
ikieleza kwa nini alichukua hatua hiyo.
Wenzake wengine katika chuo kikuu
na wenyeji walimiminika katika eneo la tukio Jumatano baada ya kupata habari
kuhusu tukio hilo.
Enjoying this article?
Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans
Polisi walifika eneo la tukio na
kuuchukua mwili wa marehemu hadi katika chumba cha kuhifadhia maiti ukisubiri
uchunguzi wa maiti na uchunguzi mwingine.
Katika barua yake, Ryan Kitari
alielezea matatizo yake ya kifedha, shinikizo la kitaaluma, kiwewe cha
kibinafsi na maisha yake ya zamani kama sababu za kuchukua hatua hiyo.
Wenzake na marafiki walijitokeza
kwenye mitandao ya kijamii kuomboleza kifo cha mwanafunzi huyo wa Chuo Kikuu.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!