
MWANAMUME mmoja mwenye umri wa miaka 30 amejikuta
kwenye njia panda baada ya mke wa marehemu babake kudhihirisha hisia za mapenzi
kwake na hata kumwandikia barua akimuarifu hilo.
Kijana huyo alieleza mafadhaiko yake kupitia kwa
mtumizi mmoja wa mitandao ya kijamii anayetoa nafasi kwa watu kueleza masaibu
yao kwa ahadi ya kutotambuliwa kwa majina yao na picha.
Alionekana kuzama katika bahari ya luja na kusimulia
kwamba anamheshimu sana mama mdogo lakini sasa hajui itakuwaje maana mama
ameshamtaarifu utayarifu wake wa kuwa katika mapenzi naye.
Alisema kwamba babake alifariki miaka 8 iliyopita, na
miaka 5 baadae, mama wa kambo akaanza kumpa ishara na dalili zote za kumtaka
kimapenzi licha ya kuwa ni mama mwenye umri wa miaka 36.
Alisimulia hivi: “Siku njema, Mkuu. Nilimpoteza baba yangu
miaka 8 iliyopita. Alikuwa na wake wawili, mama yangu akiwa mkubwa. Ninafanya
kazi katika sekta ya madini na kupata kiasi kinachostahili. Nina umri wa miaka
30, wakati mke mdogo wa baba yangu ana miaka 36 na watoto wawili (alipoteza
mmoja kwa sababu ya ugonjwa). Zaidi ya miaka mitatu iliyopita, aliniambia kwa
kawaida kuwa alikuwa akikuza hisia kwa ajili yangu na alihisi nilipaswa kujua.
Sikulichukulia kwa uzito wakati huo.”

Akifikiria ni mzaha, kijana huyo alipata mama wa
kambo amemtumia zawadi maridadi siku yake ya kuzaliwa mapema mwaka huu.
Japo alikiri kwamba si mara ya kwanza kwa mama wa
kambo kumtumia zawadi ya kusherehekea siku yake ya kuzaliwa, alisema safari hii
zawadi iliambatanishwa na barua ya kumkumbusha kuhusu hisia zake za mapenzi
kwake.
Jambo hilo lilimpiga dafrau ghafla na kujipata katika
njia panda huku akiomba ushauri wa jinsi ya kutatua suala hilo baina yake na
mke mdogo wa marehemu babake.
"Ili kufupisha kila kitu, siku yangu ya kuzaliwa mnamo Machi,
alinitumia zawadi, kama kawaida yake kila mwaka, lakini wakati huu ilikuja na
barua. Katika barua hiyo, aliandika kwamba anakufa moyoni kwa sababu hawezi
tena kudhibiti hisia zake kwangu.”

Ufichuzi wa kushtua wa mwanamume huyo ulienea haraka, huku
watu wengi waliohusika walifurika sehemu ya maoni ili kutoa ushauri.
Baadhi walimtaka kupotezea uwezekano wa kutokea kwa kitu
chochote baina yake na mke wa babake wakisema kuwa hafai hata kuendekeza hisia
za mapenzi kwa mtu aliyeonana kimwili na babake mzazi.
Walimshauri kutorudi nyumbani kabisa na ikiwezekana kukata
mawasiliano na mama wa kambo.
Hata hivyo, watoro wengine wa maadili walimtaka kudakia
fursa hiyo, wakisema kwamba pengo la umri kati yao ni miaka 6 tu ambalo kwao si
pengo kubwa.
Je, wewe una ungepata nafasi ya kuketi chini na kijana huyu, ungemshauri vipi?
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!