November 24, 2024
1 min read
Mvulana mwenye umri wa miaka 12 alifariki baada ya basi kuhusika katika ajali kwenye barabara ya Ngong, Nairobi siku ya Jumamosi.
Ajali hiyo iliyotokea Jumamosi jioni, Novemba 23, pia iliacha takriban watoto wengine 25 wenye umri wa kati ya miaka 10 na 16 wakiwa na majeraha.
Kundi hilo, ambalo ni sehemu ya timu ya soka kutoka mtaa moja eneo la Syokimau, lilikuwa likirejea nyumbani baada ya mafunzo ya kandanda kwenye Uwanja wa soka wa Talanta kando ya Barabara ya Ngong.
Kwa mujibu wa mashahidi, ajali hiyo ilitokea wakati basi dogo walilokuwa wamelikodi lilikuwa likiungana na barabara ya ICD.
Inasemekana kuwa dereva alishindwa kulidhibiti gari hilo na kusababisha kuacha njia na kugonga reli ya ulinzi na kuteremka kabla ya kutua upande wake.
Enjoying this article?
Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans
Watoto waliojeruhiwa walikimbizwa katika hospitali mbalimbali, huku 16 wakiripotiwa hali zao zinaendelea vizuri.
Msemaji wa Polisi wa Kitaifa Dkt. Resila Onyango alithibitisha maelezo hayo, na kuongeza kuwa watu wazima watatu walioandamana na watoto hao—kocha wao na walezi wawili—pamoja na dereva, pia waliripoti majeraha lakini walihudumiwa na wanaendelea kupata nafuu.
Mvulana huyo mwenye umri wa miaka 12 alifariki dunia kutokana na majeraha yake alipokuwa akipokea matibabu katika Hospitali ya jiji.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!