
Waziri Mkuu wa zamani wa Kenya Raila Odinga mnamo Alhamisi alipata fursa ya kukutana na rais wa Togo Faure Essozimma Gnassingbe huku akiendelea kuomba uungwaji mkono kwa kiti cha uenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika (AUC).
‘Nilikuwa na mashauri yenye manufaa na Rais Faure Gnassingbé wa Togo, kuhusu fursa, changamoto, na masuluhisho yanayoweza kukabili bara la Afrika,” Raila alisema kupitia akaunti yake ya X.
"Ushirikiano wangu na viongozi kote barani ni sehemu ya programu yangu ya kufikia watu ili kutafuta uungwaji mkono kwa ajili ya zabuni yangu ya Uenyekiti wa Umoja wa Afrika," aliongeza.
Rais Gnassingbe wa Togo alithibitisha kukutana na Raila na kufichua kuwa walikuwa na mijadala kuhusu hali ya kisiasa na usalama barani Afrika.
‘Rais wa Jamhuri, @FEGnassingbe mnamo Alhamisi, Novemba 21, 2024, amekutana na Waziri Mkuu wa zamani wa Kenya, @RailaOdinga.Miongoni mwa mada za ni, hali ya kisiasa na kiusalama barani Afrika pamoja na changamoto za maendeleo ya kiuchumi na kijamii. barani,” ikulu ya Togo ilisema.
Uchaguzi wa Tume ya Umoja wa Afrika utafanyika Februari 2025 na Raila Odinga amekuwa akisafiri kote barani Afrika akijipigia debe na kuomba kuungwa mkono.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!