Kamati ya dharura ya Shirika la afya duniani (WHO) imethibitisha kuwa Mpox inasalia kuwa dharura ya kiafya ya umma kimataifa (PHEIC)
Hii ni tahadhari kubwa iliowahi kutolewa kwa mlipuko wowote ule uliowahi kutokea. Mkurugenzi mkuu wa WHO, Tedros Ghebreyesus, ameidhinisha mapendekezo ya kamati hiyo akitaja visa vinavyoongezeka, kusambaa kwa ugonjwa huo katika maeneo mapya na uhitaji wa dharura wa kuwepo muitikio ulioratibiwa kimataifa.
Ripoti kamili ya mapendekezo ya kamati hiyo inatarajiwa kuchapishwa wiki ijayo.
Visa vya Mpox vimekuwa vikiongezeka Afrika mashariki na kati tangu mapema 2024 huku Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo ikiathirika pakubwa na aina mpya na kali ya ugonjwa huo ijulikanayo kama Clade 1b.
Hii ilichangia tangazo la awali mnamo Agosti la dharura ya kiafya ya umma kimataifa. Mpaka sasa nchi 20 za Afrika zimeripoti visa vya maambukizi huku Angola ikiwa ndio nchi ya hivi karibuni kuripoti maambukizi.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!