KAMPUNI ya kusambaza umeme nchini Kenya (KPLC) imeonya kuhusu kukatizwa kwa umeme katika maeneo kadhaa nchini siku ya Jumamosi Novemba 23.
Katika kaunti ya Kisumu, eneo la soko ya Riat litaathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa sita adhuhuri.
Maeneo ya Kisumu Poly na Manyatta yatakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.
Katika kaunti ya Siaya, maeneo ya Tingwangi, Anduro na Malanga yataathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa mbili asubuhi na saa kumi na moja jioni.
Maeneo ya Pap Kadero na Madiany pia yataathirika kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!