
SENETA maalum Karen Nyamu amezua utani kwenye
mitandao ya kijamii jinsi inbox zake zimefurika baada ya kudaiwa kwamba ana
deni la mwenye nyumba yake.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Nyamu alichapisha
picha yake akidai kwamba kuna watu wanaojidai kuwa waganga ambao wamejaza inbx
yake kwa jumbe za kutaka kumpa msaada.
Seneta huyo wa UDA alisema kwamba wengi wao wanajidai
kuwa waganga wakimtaka kutuma shilingi elfu 20 na picha ya mlango wa nyumba
yake ili waipigie ramli ya kumfanya mwenye nyumba kusahau kama anamdai.
“Ati
nauza dawa ya kufanya landlord asahau rent, tuma tu 20k na picha ya mlango wako??♀️??♀️ Hawa waganga kutaka
kulipua inbox yangu jameni,” Karen Nyamu alisema.
Kauli hii inajiri siku moja tu baada ya vyanzo vya
habari humu nchini kudai kwamba mali ya Karen Nyamu huenda ikawekwa kwenye soko
la mnada baada ya kukosa kulipa kodi ya nyumba.
Inaripotiwa kwamba Nyamu anadaiwa kodi ya nyumba ya
hadi shilingi milioni 1.25 na mwenye nyumba wake.
Hata hivyo, Nyamu akizungumza katika kituo kimoja cha
runinga humu nchini Jumanne, alipuuzilia mbali madai hayo akisema kwamba yeye
na mwenye nyumba wake wako katika maelewana mazuri.
Pia alifichua kuwa baadhi ya watu wanatumia mbinu za
siri kujaribu kumshinikiza afanye mambo ambayo hakutaja.
"Kuna
watu wanaofikiri wanaweza kufadhili vyombo vya habari, kutumia njia za kihuni
kukupotosha na kukutisha, na kwenda kwenye matakwa ili kutoa ahadi ambazo
wanajua kabisa si sahihi," alisema.
Alifunga mjadala, na kuongeza kuwa hayuko tayari
kushughulikia maswala yake hadharani.
"Na
niko hapa kuwafundisha haifanyi kazi na kila mtu. Njia sahihi lazima ifuatwe na
sitaki kushughulikia masuala yangu hadharani,”
alisisitiza.
Nyamu hata hivyo alifichua kwamba baada ya ripoti za
kudaiwa kodi ya nyumba kusambaa, alipokea hela kadhaa kwenye simu yake kutoka
kwa watu lakini akasema hahitaji michango zaidi.
"Kwa
kweli nilipata michango kwenye simu yangu na ninashukuru Wakenya lakini
sijambo, sihitaji michango sasa."
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!