
NYOTA wa UFARANSA,
Ousmane Dembele tayari amepanga kustaafu licha ya kuwa na umri wa miaka 27
pekee.
Dembele tayari amepata
mafanikio makubwa katika klabu zote mbili na hasa ngazi ya kimataifa, baada ya
kushinda Kombe la Dunia la 2018 akiwa na Les Bleus.
Mshambulizi huyo pia
anahesabu mataji matatu ya LaLiga pamoja na mataji mawili ya Copa del Rey akiwa
na Barcelona, Kombe la Ujerumani akiwa na Borussia
Dortmund na mara mbili msimu uliopita akiwa na klabu ya sasa ya Paris
Saint-Germain.
Na Dembele anaonekana
kuwa amebakisha takriban miaka saba tu katika maisha yake ya soka kushinda tuzo
nyingi zaidi.
Hiyo ni kwa sababu
mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa alifichua kuwa ataamua kutundika daruga
zake za soka akiwa na umri wa miaka 34.
Na kisha nyota huyo wa
zamani wa Rennes anapanga kuingia katika biashara ya mali isiyohamishika nchini
Ufaransa pamoja na mataifa kadhaa ya Afrika.
Dembele aliliambia The
Bridge - kipindi cha YouTube, ambacho kimetolewa na mchezaji mwenza wa Real
Madrid na Mfaransa Aurelien Tchouameni: "Nataka kustaafu nikiwa na umri wa
miaka 34.
"Na kisha nataka
kuingia katika biashara ya kumiliki mali. Wekeza Afrika, nchini
Ufaransa..."
Dembele ameanza vyema
PSG msimu huu kwani tayari ana mabao matano na asisti saba katika mechi 13 za
michuano yote.
Tangu alipowasili Paris
akitokea Barcelona mwaka jana, mshambuliaji huyo mahiri ana jumla ya mabao 11
na asisti 21 katika mechi 55.
Mfaransa huyo pia
amesajili jumla ya mabao sita na asisti nne katika mechi 53 alizocheza na timu
yake ya taifa.
Hiyo ni pamoja na mechi
nne katika Kombe la Dunia miaka sita iliyopita, wakati Ufaransa iliponyanyua
kombe hilo.
PSG watarejea uwanjani
Ijumaa kwenye Ligue 1 dhidi ya Toulouse huko Parc des Princes.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!