Saa chache baada ya msanii Willy Paul kumuomba Bahati
na familia yake msamaha kwa mifarakano ya awali iliyoishia mahakamani, Bahati
amevunja kimya chake.
Akichukua kwenye ukurasa wake wa Instagram, Bahati
alichapisha picha ya zamani wakiwa pamoja na Willy Paul wakati wanahangaika
kutoboa tundu kwenye Sanaa ya injili.
Alianza kwa kukubali msamaha wake na kumkumbusha
jinsi walikuwa wanahangaika juu chini katika mtaa duni wa Mathare enzi za
nyuma.
Alimalizia kwa kumtaja kama ‘kaka wa milele’ na
kusema kwamba Mungu ni wa nafasi ya pili, huku akimshauri kuungana naye
kuendeleza Sanaa badala ya kuendeleza bifu.
“Ndugu
Yangu @willy.paul.msafi ,Msamaha Umekubaliwa ?
Tumetoka mbali, Sote tumepambana na changamoto nyingi na umasikini mkubwa
katika Vitongoji duni vya Mathare ili kuwa hivi tulivyo leo na tunapojitahidi
kuinuka na kuwa wakuu katika njia tumefanya makosa mengi lakini cha muhimu ni
kurudi nyuma na kurekebisha pale tunapofikiri tulikosea kwani Mungu wetu ni Mungu
wa Upendo na nafasi ya Pili. Zaidi ya yote hakuna kosa kubwa kuliko udugu
tunaoshiriki,” Bahati alisema.
Awali, Willy Paul alichapisha picha ya familia nzima
ya Bahati, na kuandika ujumbe akijuta jinsi alijipata katika hali ya
kukorofishana na Diana Marua.
Alichukua fursa hiyo kuomba msamaha Diana na watoto
kwa kile alichokitaja kuwa ni kuwaingiza katika zogo lake na Bahati.
“Nikikumbuka
mambo niliyojionea na kaka yangu, ninatambua kwamba mara kwa mara nimevuka
mipaka. Ninashikilia sana dhana ya familia, haswa watoto. Matendo yangu hayakukusudiwa
kamwe kusababisha madhara, lakini ninaelewa kwamba yalionekana hivyo, na
ninaomba msamaha kwa Diana na watoto Kwa Upendo wa Kutokuelewana,”
Willy Paul aliandika.
Itakumbukwa Willy Paul na Diana mnamo 2021
walipapurana vikali kwenye mitandao ya kijamii wakishushiana shutuma mbaya
ambazo zilitishia kusambaratisha kabisa maisha ya Sanaa ya kila mmoja wao.
Diana alirekodi video akihadithia baina ya vilio kile
alichodai kuwa ni kudhulumiwa kingono na Willy Paul, jambo ambalo Pozee
alielekea mahakamani akidai ni kuchafuliwa sifa.
Mahakama ilimuamuru Marua kufuta video ile mara moja
huku kesi hiyo ikijikokota mahakamani hadi hivi majuzi ambapo Pozee alifichua
kuwa madai dhidi yake yametupiliwa mbali.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!