Msanii na mjasiriamali Esther Akoth maarufu kama Akothee amemkaripia kwa ukali wa simba bukaa aliyejeruhiwa, jamaa mmoja aliyejaribu kumpa ushauri kuhusu jinsi ya kujibeba akiwa na mpenziwe wake katika mazingira ya umma.

Mjasiriamali huyo ambaye kwa zaidi ya wiki sasa yuko nchini Uganda na mpenzi wake Nelly Oaks alichapisha msururu wa picha kadhaa wakiwa katika hali ya tafrija kwenye mto Nile.

Katika picha hizo, Akothee na Nelly Oaks walikuwa wakicheza densi kwa furaha huku zingine wakiwa wamepakatana na kubusiana kwa mahaba hai.

Mtumizi mmoja wa Facebook alionekana kutofurahishwa na picha hizo, haswa za wawili hao kubusiana na kumpa Akothee funzo kuhusu baadhi ya mambo ambayo hafai kuyaonyesha hadharani.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Kwa mujibu wa jamaa huyo, Akothee katika umri wake hafai kufanya mambo kama ya kubusiana hadharani na mpenzi wakwe, akiitaja kama tabia mbaya.

Hata hivyo, Akothee naye hakutaka kumweka mfungwa, alimkabili moja kwa moja akimsuta kwa kuingilia maisha yake.

Sasa wewe na mimi nani ako na tabia mbaya, I have been kissed on camera ,wewe bibi yako ushamtia mimba tayari , sasaaa si hata sisi uwache tutafute mimba style yetu? Nyinyi ni wa usiku muonekane mchana, sisi ni wa mchana na usiku tuko bisi,” Akothee alimzomea.

Akothee alizama zaidi hadi kuipata picha ya jamaa huyo akiwa na mwanamke aliyeonekana kama mpenzi wake na kuitumia kumshambulia zaidi, akimwambia kuwahata yeye kuchapisha picha na mkewe mjamzito hakuna tofauti na yeye [Akothee] kuchapisha picha akimla denda Nelly Oaks.

“Hivyo wewe unahisi kuchapisha picha ya mpenzi wake akiwa mjamzito ni tabia nzuri lakini mimi kuchapisha picha nikimbusu mpenzi wangu ni tabia mbaya? Eeeeh watu waache kupangie wengine maisha. This is one is a coward cant even hold the wife in public ,anangoja giza. Weeee mimi siogopi mtu,” Akothee alimfokea.

Hata hivyo, Akothee si mgeni kwa majibu yake makali kwa watu mitandaoni ambao wanajaribu kuingilia maisha yake au kutaka kumpa ushauri.

Yeye na Nelly Oaks walirudiana mwaka jana baada ya kuachana kwa zaidi ya mwaka mmoja.

Nelly Oaks alirejea katika maisha ya mfanyibiashara huyo baada ya penzi lake na Mzungu kusambaratika miezi michache baada ya kufanya harusi iliyotikisa nchi mnamo Aprili mwaka jana.