Mwanasosholaiti Huddah Monroe amemmiminia sifa mbunge wa Embakasi Mashariki, Paul Ongili maarufu kama Babu Owino, akifichua kuwa ndiye chanzo cha utajiri alio nao kwa sasa.

Monroe alichapisha msururu wa jumbe za kumvisha koja la maua Babu Owino akisema kuwa ndiye aliyekuwa mtu wa kwanza kumtoa mitaani na kumuonyesha njia za kutafuta pesa.

Huddah alisimulia kwamba alikuwa ni maskini wa kutupwa hadi wakati alipokutana na Babu Owino ambaye alimshika mkono na kumuonyesha jinsi ya kutafuta pesa na utajiri.

“Nilikuwa nikihangaika, yaani sikujua kodi inayofuata ingetoka wapi. Sijui ni jinsi gani au ni nani aliyenitambulisha kwa Babu Owino enzi hizo. Niliishi kwenye nyumba ya chumba kimoja hapo Kile. Barabara ya Kandara.”

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

“Babu ananipigia simu siku moja, ananichukua kwenye Benz! Ndio jamaa alikuwa na Benz siku hizo. Nadhani aliweza kusema kuwa nilikuwa najitahidi kweli! Akaniuliza ‘umechoka kuishi mkono kwa mdomo?’ Je, hata mimi nilikuwa naishi? Tuliendesha gari karibu na Arboretum na akanionyesha jinsi ya kutengeneza sarafu! Mengine ni historia! Lakini alifungua macho yangu ya umaskini,” Huddah alisimulia.

Mrembo huyo ambaye siku za hivi karibuni ameonekana kuwa mstari wa mbele kuzungumzia hali ya uchumi wa Kenya chini ya utawala wa rais William Ruto, alisema hata hivyo urafiki wake wa muda mrefu na Babu Owino ulikatika miaka michache iliyopita.

Huddah alifichua kwamba alianza kumuona Babu Owino kwa taswira tofauti baada ya kuhusishwa na tukio la kumfyatulia risasi mcheza santuri DJ Evolve katika klabu moja ya starehe mtaani Kilimani miaka michache iliyopita.

Huddah alisema kwamba hajui tukio hilo alilaumu kwa Babu Owino au kwa ulevi.

“Tulikosana alipompiga risasi yule kijana labda ilikuwa pombe, kusema kweli maji ya mashetani yanaweza kukupelekea kufanya dhambi za kichaa. Lakini ndani ya roho yake, Babu Owino ni mtu mzuri. Hataona vijana wakihangaika wala jiji likigeuka kuwa makazi duni na anyamaze,” Huddah alimpaisha Babu.

Babu Owino, mtetezi mkali wa sera za chama cha ODM amekuwa akihusishwa kujitosa katika kinyang’anyiro cha ugavana katika kaunti ya Nairobi mwaka 2027 ambapo huenda akamenyana na gavana wa sasa, Johnson Sakaja.