
Muigizaji Jacky Matubia amefichua kwamba maisha yake
ya utotoni yalikuwa na kiwewe kisichoweza kuelezeka kutokana na tofauti kati ya
wazazi wake.
Mama huyo wa mabinti 2 alisema kwamba alimchukia mama
yake sana baada ya kugundua kwamba alimzaa katika hospitali ya kujifungua kina
mama ya Pumwani na kumtelekeza huko kwa miezi 3.
Matubia alisema kwamba maisha yake yote ya utotoni
yalikuwa ya kutojikubali, jambo ambalo linamtatiza mpaka sasa.
Ilikuaje?
Kwa mujibu wa muigizaji huyo, kulikuwa na tofauti za
kutoelewana kati ya babake na mamake, jambo ambalo alisema kuwa mpaka sasa
hawajahi zungumza wala kuonana ana kwa ana.
“Niliishi
London kwa miezi 6 na babangu kabla ya kurudishwa kwa mamangu Kawangware. Mama alipigana
sana kunilea. Mimi binafsi nilikuwa namchukia sana mamangu. Nilikuwa najiuliza
mbona unilete duniani kama ulikuwa unajua nitakuja kuteseka,”
Matubia alisema.
“Mamangu
na babangu hawazungumzi mpaka leo hii nikiwa na umri wa miaka 34. Hawajawahi onana.
Kutojikubali kwangu kulianza wakati mamangu alinizaa. Aliniacha Pumwani kwa
miezi 3 bila mlezi kwa sababu aliambiwa mimi ni sura mbaya. Nilikuwa mweusi na
nywele nyingi,” aliongeza.
‘Hivyo ni kama nilizaliwa tu kwa kujikataa na limekuwa
ni jambo ndani yangu.”
Akiwa katika shule ya upili, Matubia alisema hapo
ndipo alianza kujitambua kwa sababu alipelekwa katika shule ambayo iliwiana na
hali ya uchumi ya mama yake.
Matubia alisema kuwa baada ya kumaliza kidato cha
nne, alipata kazi yake ya kwanza ya uigizaji kwenye Tahidi High ambapo mshahara
wake wa pili alihama kutoka kwa mamake Kawangware na kuishi Imara Daima.
Akizungumzia kuhusu alichokifunza kutoka maisha yake
ya utotoni, Matubia alisema yeye si bahili wa kutumia pesa, akisisitiza kwamba
asingependa kuwakuza wanawe katika maisha sawia na yale aliyopitia.
“Nisingependa kurudi kule nilikokuwa. Nisingependa hata kidogo kuwalisha wanangu ugali na chai pekee. Na ndio maana ninafanya kazi kwa bidii. Nimeamua kupumzika itakuwa ni mbinguni;” alisema.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!