Mchungaji Robert Burale amefichua kwamba amepitia mapito mengi sana katika mitandao ya kijamii, yote yakilenga jinsi anavyojibeba.

Akizungumza kwenye podikasti ya Lessons At 30 na mkuza maudhui maarufu, Dr Ofweneke, Burale alisema kwamba ilimchukua kipindi cha miaka 3 kuwa na ukakamavu wa kutobebwa na kauli hasi za watumizi wa mitandao ya kijamii.

“Ilinichukua miaka 3 kuwa mkakamavu kwa maoni hasi mtandaoni. Maoni mabaya zaidi nimewahi kuyaona kuhusu mimi, siwezi hata weka kidole kwayo lakini kwa wakati Fulani kuna mtu alijaribu kumshambulia binti yangu.”

“Nilimwambia mtu huyo kwamba sitomuendea nikiwa kama Pastor Burale bali ningemwendea kama Robert na aliomba msamaha,’ Burale alisema.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Alifichua kwamba kuna baadhi wamekuwa wakijaribu kumshambulia kutokana na chaguo la rangi ya mavazi yake muda wote.

Burale alifichua kwamba aliwahi itwa mchungaji wa iluminati kutokana na upendo wake kwa mavazi ya rangi nyeusi.

“Wenye chuki hawawezi kusema chochote cha hakika, kuna mtu aliniita pasta wa iluminati eti ndio maana nahubiri nikiwa nimevaa nguo nyeusi. Ukweli ni kwamba mimi napenda nguo nyeusi na nitaendelea kuvaa nguo nyeusi. Mimi navaa suti nyeusi na hata boxer nyeusi, ni vile tu siwezi onyesha,” Burale alisema.

Burale alisema kwamba matukio kama hayo yamemfanya kubana idadi ya marafiki zake, akisema kuwa yeye ana marafiki 4 tu.

“Babangu alikuwa anatumia vitabu viwili kunifunza; Biblia na kitabu cha Shakespear. Aliniambia kwamba mwanangu usiwe na marafiki wengi. Kuwa mkarimu kwa kila mtu lakini usikuwe rafiki wa kila mtu. Kusema kweli mimi huwaambia watu kama uko na marafiki zaidi ya 5 unafaa kuenda kukaguliwa kichwa chako. Mimi marafiki zangu wakienda sana ni 4,” Burale alisema.

Mchungaji huyo alisema kuwa marafiki katika mzunguko wa maisha yake ni wa kategoria nne; marafiki wa maeneo ya kuegesha gari, marafiki wa sebuleni, marafiki wa jikoni na mawafiki wa chumbani.

“Mimi huwa makini sana kuhusu ni nani ninakubalia kuingia katika nafasi yangu. Ndio maana nasema kuna marafiki wa maegesho ya magari, kuna marafiki wa sebuleni, kuna marafiki wa jikoni na kuna marafiki wa chumbani.”

“Marafiki wa maegesho ya magari ni wale ambao mnaweza jadili kitu chochote huko nje, marafiki wa sebuleni ni wale ambao unakubali kuingia kwako na muwe na mazungumzo ya kina na hata kutoka kwenye ziara nao, marafiki wa jikoni ni wale unaweza kuamini kwa sababu jikoni kuna kisu, watu ambao hawawezi kukuchoma mgongoni na marafiki wa chumbani ni wale ambao unaweza ukaamini na siri zako za ndani ambazo zinaweza kufanya kuwa mdhaifu lakini hawawezi kukuabisha,” mchungaji huyo alisema.