
Leo hii, Novemba 14, mtoto wa kwanza wa seneta Karen Nyamu na mwimbaji Samuel Muchoki almaarufu Samidoh anaadhimisha siku yake ya kuzaliwa.
Samwel Muchoki Jr alizaliwa miaka minne iliyopita, siku kama hii na seneta Nyamu ametumia siku ya leo kusherehekea tunda la pili la tumbo lake.
Katika ujumbe wake kwa mwanawe, seneta huyo wa kuteuliwa alitumia mstari wa Biblia kutoka Zaburi 112:2 kueleza umaana wa watoto.
“Watoto wao watakuwa hodari katika nchi, kizazi chao kitabarikiwa - Zaburi 112:2. Tafadhali nisaidie kumtakia kijana huyu mwema siku njema ya kuzaliwa kwa 4,” Karen Nyamu aliandika kwenye Facebook.
Aliambatanisha taarifa yake na picha mbili nzuri za mtoto wake.
Aliendelea kuelezea sifa za mwanawe na kuelezea jinsi anavyoathiri maisha yao vizuri.
"Ni sauti zako tamu, zisizo na hatia lakini bado ni za kihuni na za kihuni. Ni ucheshi wako na jinsi unavyocheka vicheshi vyako hadi sote sasa tunacheka kicheko chako.
Ni jinsi unavyoniabudu na jinsi unavyotabasamu kwa macho yako. Lazima uwe umepata haiba yako kutoka kwa mama yako ?,” alisema.
Mwanasiasa huyo ambaye pia ni wakili pia alitaja kuhusu mapenzi yake mengi kwa mtoto wake wa pili.
"Wewe ni zawadi ya thamani kwetu. Tunakupenda sana baby. Happy birthday baby Samwel Muchoki jr??,” alisema.
Samwel Muchoki Jr ni mtoto wa kwanza wa Karen Nyamu na mpenzi wake wa hivi majuzi Samidoh. Haijabainika vyema iwapo wawili hao bado wako kwenye uhusiano au wametengana.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!