
Mwanasosholaiti Huddah Monroe amejitokeza wazi na
kukiri kwamba anajionea huruma kwa kile alichokitaja kuwa ni kumpigia rais Ruto
debe kuelekea uchaguzi mkuu wa Agosti 2022.
Kupitia Insta story yake, Monroe alisema kwamba
anajuta kitendo hicho akidai kuwa rais amefeli katika maazimio yake mengi
aliyowaahidi Wakenya katika manifesto yake.
Mwanasosholaiti huyo alisema kwamba mtambo wa KRA uko
na hitilafu kila mara kuifanya kuwa vigumu walipa ushuru kutekeleza wajibu wao,
akiwashauri Wakenya kutompa ‘mtoto wa maskini’ wajibu wa kuwaongoza tena.
“Mitambo
ya KRA ina hitilafu kila mara, Kenya imekuwa kama kichaka kikubwa. Ni kijiji tu
ndichi kinastahili kuwa na matatizo kama haya. Sasa mmejua, msiwahi kumpa
uongozi mtoto wa maskini tena. Pengine tu kama amejenga biashara yake
iliyostawi,” Monroe alisema.
“Niliweka
ubashiri mbaya! Mimi ni miongoni mwa watu waliompigia debe bila aibu,’
Huddah aliongeza.
Katika siku za hivi karibuni, mwanasosholaiti huyo
ambaye mara nyingi hayuko nchini amekuwa akijiingiza katika masuala ya uongozi
wa Kenya, kinyume na awali ambapo alikuwa amejikita katika kutangaza biashara
zake kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii.
Hii si mara ya kwanza ambapo sosholaiti huyo alikosoa
utawala wa Rais Ruto.
Huku kukiwa na kupanda kwa bei ya mafuta na vyakula
mnamo Septemba 2023, Huddah alionyesha kutoridhika kwake, akidai kwamba Ruto
atakumbukwa kama rais mbaya zaidi wa Kenya.
Ikumbukwe Monroe alikuwa mmoja wa watu maarufu kwenye
mitandao ya kijamii ambao walionyesha wazi uungaji mkono wao kwa Ruto tangia
mwaka wa 2017 akiwa naibu rais wa aliyekuwa rais, Uhuru Kenyatta.
Wakati Ruto alishinda katika uchaguzi wa urais wa
2022, Huddah alikuwa miongoni mwa wa kwanza kusherehekea, akishiriki picha
nyingi za kiongozi wa taifa akichapisha picha zake kwenye Instagram, ambapo
alimtaja kama "rais wangu."
Alionyesha hisia mpya ya fahari ya kitaifa.
“Ninajivunia kuwa Mkenya kuanzia leo. Afrika
inastahili viongozi wenye nguvu, wenye akili timamu, vijana. Kenya imefanya
mabadiliko kwa Afrika. Nitabeba bendera na pasipoti yangu kwa fahari kuanzia
leo. Ninatoka Kenya, nchi kubwa zaidi barani Afrika!” Alisema.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!