
Heaven Bahati, binti wa kwanza wa maceleb Diana Marua
na Kevin Bahati Kioko amefichua mipango yake ya ni lini ataondoka katika nyumba
ya wazazi.
Akizungumza na wazazi wake wakati aliwaandalia zawadi
ya kuwashukuru kwa malezi, binti huyo aliwaambia Bahati na Diana kwamba mpango
wake ni kuondoka chini ya mbavu zao afikapo umri wa miaka 21.
Binti huyo mwenye umri wa miaka 7 alisema kwamba
kabla hajaondoka, atachukua picha nzuri za wazazi wake zitakazosalia naye kama
kumbukumbu ya milele katika moyo wake ili asije akawasahau.
“Siwezi
kuwasahau hata wakati nitaenda katika nyumba nyingine. Ninapanga kuenda katika
nyumba yangu nikifikisha umri wa miaka 21.”
“Lakini
nitakuwa ninawaweka moyoni milele, nitachukua picha zenu nzuri na nitazitunza
kwangu muda wote. Nitafanya hivyo kama njia moja ya kuhakikisha siwapotezi
katika moyo wangu,” binti huyo alieleza kwa hisia.
Binti huyo mrembo aliwamiminia wazazi wake sifa,
akisimulia jinsi wanafanya kazi kwa bidii kuhakikisaha familia yao hailali
njaa.
“Ninawathamini
kwa sababu nyinyi ni wazazi 2 mnaofanya kazi kwa bidii kulisha familia ya
watoto 5. Mama anakuwa kila wakati akifanya vitu vingi vizuri kwa ajili yetu,
hata kama tunakosea, tunafoka. Lakini pia baba anafanya kazi sana, anasafiri
sana mpaka kwa muda sasa hatujakuwa tukimuona kwa sababu amekuwa safarini
akitusaidia kupata pesa,” Binti Heaven alisema.
Hii si mara ya kwanza kwa binti huyo kuwapunga wazazi
wake kwa mawazo yake kuhusu maisha yake ya kibinafsi.
Itakumbukwa mwezi Julai mwaka huu, Heaven Bahati
alimuacha mamake kinywa wazi baada ya kumuonyesha pete yake vya uchumba, akiwa
na umri wa miaka 6.
Diana alikuwa amejiandaa kutoka kukutana na
baadhi ya mashabiki wake na kusherehekea kupokezwa Kitufe ch Dhahabu kutoka
YouTube baada ya kufikisha wafuasi milioni 1 mapema mwezi Februari mwaka huu.
Diana alikutana na bintiye nje na kumuonesha pete zake mbili akimfafanulia bintiye kwamba moja ni ya urembo na nyingine ni ya kuonyesha uhusiano wake wa kimapenzi na mumewe, Bahati Kioko.
Kwa mshangao, Heaven pia alimuonyesha mama yake pete mbili kwenye vidole vyake mkononi na kusema moja ni ya urembo na nyingine ni kwa ajili ya ‘mumewe’, akisema kwamba yuko tayari kuolewa siku wazazi wake watamruhusu kutoka bila kuomba ruhusa.
“Kwa sasa nimeolewa na watu wawili,” Heaven Bahati alisema kabla ya mamake
kumkatisha na kumwambia kwamba angependa aje kuolewa na mtu mmoja baadae
mbeleni.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!