
Mahakama ya Uturuki
imemhukumu mtendaji wa zamani wa klabu ya soka ya daraja la juu kifungo cha
zaidi ya miaka mitatu na nusu jela siku ya Jumatatu kwa kosa la kumshambulia
mwamuzi uwanjani mwishoni mwa mchezo wa ligi msimu uliopita.
Rais wa zamani wa
Ankaragucu, Faruk Koca alimpiga mwamuzi Halil Umut Meler ngumi usoni baada ya
firimbi ya mwisho ya sare ya 1-1 katika mchezo wa Super Lig dhidi ya Caykur
Rizespor mwaka jana.
Meler, ambaye alianguka
chini, pia alipigwa teke katika vurugu iliyotokea wakati mashabiki pia
walipovamia uwanja baada ya Rizespor kufunga bao la kusawazisha dakika ya
mwisho mnamo Desemba 11, 2023.
Tukio hilo lilikuwa
limezua ghadhabu duniani na kulifanya Shirikisho la Soka la Uturuki kusimamisha
michezo yote ya ligi kwa wiki kadhaa.
Mahakama mjini Ankara
ilimtia hatiani Koca kwa "kumjeruhi kwa kukusudia afisa wa umma" na
kumhukumu kifungo cha miaka mitatu na miezi saba jela, Shirika la serikali la
Anadolu liliripoti.
Mahakama hiyo pia
ilimtia hatiani Koca kwa kosa la kumtishia mwamuzi na kukiuka sheria
zinazolenga kuzuia vurugu michezoni lakini ikamsimamisha adhabu hiyo.
Watu wengine watatu
ambao pia walikuwa kwenye kesi ya kumshambulia mwamuzi, walihukumiwa vifungo
vya kuanzia mwaka mmoja hadi mitano, shirika hilo liliripoti.
Koca, ambaye alijiuzulu
kama rais wa klabu mara baada ya tukio hilo, anatarajiwa kukata rufaa dhidi ya
uamuzi huo. Alifungwa kwa muda mfupi mwaka jana kabla ya kuachiliwa kwa
dhamana.
Hapo awali, mawakili
wanaowawakilisha washtakiwa waliomba kuachiliwa kwao, wakidai kuwa walifanya
uhalifu huo chini ya "chokozi zisizo za haki," Anadolu aliripoti.
Ankaragucu ilipigwa faini ya milioni 2 Lira ya Uturuki ($59,000) na kulazimishwa kucheza mechi tano za nyumbani bila mashabiki.Mwamuzi huyo alilazwa kwa muda mfupi hospitalini akiwa na jeraha ndogo karibu na jicho lake.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!