
Mwanaharakati wa elimu ya kiraia, Morara Kebaso ameonyesha sura nzuri ya mkewe kwa mara ya kwanza kwa mashabiki na wafuasi wake kwenye mitandao ya kijamii.
Kebaso, akisherehekea
ndoa yake, alifichua kwamba amedumu kwenye ndoa na mrembo huyo kwa miaka 6
sasa.
Akizungumzia kuhusu
uzoefu wake kwenye ndoa, kiongozi huyo wa chama cha INJECT alieleza kwamba japo
amekaa katika ndoa kwa miaka 6, kwake kila siku huhisi kama ni mpya katika ndoa
yake.
“Apataye mke apata kitu
chema, naye ajipatia kibali kwa Bwana. Nina miaka sita kwenye ndoa sasa na kila
siku ni siku mpya. Siwezi hata kusema nina uzoefu. Ninajifunza kila siku,’
Kebaso alisema.
Wiki chache zilizopita,
Kebaso alisherehekea kufikisha umri wa miaka 29, kumaanisha kwamba alifunga
ndoa akiwa katika umri wa miaka 23.
Alipata umaarufu kote
nchini kupitia ukosoaji wake wa kuchekesha wa miradi ya serikali iliyokwama
kote nchini.
Hivi majuzi, Kebaso
aliapa kuendelea na ukosoaji wake dhidi ya serikali licha ya upinzani ambao
amekuwa akikabiliana nao siku za hivi karibuni.
Morara amelazimika kukabiliana na ukosoaji, haswa kutoka kwa mtandao wake, ambao wengine wamemwita tapeli baada ya kuanza kuomba pesa za kuwezesha harakati zake kote nchini.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!