Duru ndani ya serikali ya Urusi zinaendelea kutathmini namna gani ushindi wa Donald Trump utakavyoathiri vita nchini Ukraine.
Shirika la Habari la Urusi, Interfax limeripoti kuwa naibu waziri wa mambo ya nje wa nchi hiyo, Sergei Ryabkov, amesema kwa sasa Moscow na Washington "zinapeana ishara kuhusu Ukraine" kwa kupitia mawasiliano ya siri.
Kiongozi huyo amesema pia hakuna matayarisho yalionza kufanyika juu ya mazungumzo ya simu baina ya Rais Vladimir Putin na rais mteule Trump, lakini amedokeza kuwa Urusi ipo tayari kumsikiliza mapendekezo ya Trump ya namna ya kumaliza mzozo wa Ukraine.
Hata hivyo, Ryabkov ametahadharisha kuwa mapendekezo mengi ya Trump kufikia sasa yanaonekana kuwa kama ahadi za kampeni.
"Nafikiri baadhi ya ujumbe wake… kuhusu maazimio ya haraka sana juu ya kumaliza kinachoendela Ukraine hayana uzito… zaidi ya kuwa ni njia ya kujipatia umaarufu wakati wa kujiandaa na uchaguzi."
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!