Manchester City walikuwa mbioni kuweka rekodi ya kushinda mechi 27 bila kupoteza lakini wakaonyeshwa kivumbi mikononi mwa Sporting CP.

Sporting CP iliwanyeshea kibano cha mabao 4-1 na kumaliza msururu wao wa ushindi kwa mechi 26.

Wiki mbili zilizopita, Man City walivunja rekodi iliyokuwa inashikiliwa na Man Utd ya kuenda mechi 25 bila kushindwa kwenye mechi za bara Ulaya.