Takriban watu 10 wameuawa baada ya volkeno kulipuka mashariki mwa Indonesia mapema Jumatatu, maafisa wamesema.

Mlima Lewotobi Laki-laki, ulioko kwenye Kisiwa cha Flores katika jimbo la Nusa Tenggara Mashariki, ulilipuka saa 23:57 kwa saa za huko, kulingana na Kituo cha Kukabiliana na Volkeno na Maafa ya Kijiolojia Indonesia.

Hadi Wijaya, msemaji wa Kituo cha Kukabiliana na Volkeno, alisema lava na mawe ya moto yaliruka hadi katika vijiji hivyo takriban kilomita 4 kutoka kwenye volkeno, na kuteketeza na kuharibu nyumba za wakazi.

Kulingana na viongozi wa eneo hilo, mlipuko huo umeathiri vijiji saba.


Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans