
Kupitia Instagram yake, Khaligraph Jones alichapisha picha yake wakiwa na Samidoh na kuiambatanisha na kidokezo hicho.
Alifichua kwamba mipango yote kama itaenda sawa, basi mashabiki wao watarajie ngoma kabla ya kukamilika kwa mwaka huu, ikiwa imesalia miezi miwili tu kuuaga 2024.
“Kabla mwaka uishe Tunawapikia mugithii na @samidoh_muchoki , mtanijua nyinyi #respecttheogs,” Khaligraph Jones aliandika.
Ikiwa watafanikisha ngoma hiyo, Samidoh atakuwa amefanya kolabo ainati nje ya muziki asili wa Mugithi, kwani hapo awali ameshirikiana na wasanii mbalimbali kuachia ngoma zenye ladha mpya.
Mwaka jana, waliachia ngoma na mkali wa Ohangla, Prince Indha, ambayo ilileta ladha ya Rhumba ya kisasa kwa kuchanganya ohangla na Mugithi.
Wengi sasa wanasubiria kuona kolabo yake na Khaligraph Jones itakuwa nacladha gani, ikizingatiwa kwamba msanii huyo ni wa hiphop na yeye ni wa Mugithi.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!