Katika kisa cha kushangaza, mwanamke mmoja katika wilaya ya Tororo nchini Uganda aliwaongoza maafisa wa polisi hadi katika nyumba ya jamaa mmoja na kupata bunduki haramu iliyofichwa humo.

Kwa mujibu wa msemaji wa polisi nchini humo, mwanamke huyo kwa jina Josephine Nyapendi alidai kwamba aliletewa maono ndotoni na roho mtakatifu kuhusu bunduki hiyo haramu nyumbani kwa jamaa kwa jina Vincent Emodo.

Na kweli kwa maneno yake, baada ya kuwaongoza polisi hadi katika nyumba ya Emodo ambapo bunduki hiyo ilipatikana chini ya kitanda na kupelekea kukamatwa kwake.

“Taarifa hizo zilitolewa na Nyapendi Josephine ambaye alidai kuwa aliingiwa na roho mtakatifu hivyo kumfanya afichue uwepo wa bunduki hiyo kwa Onyapidi Alfonse aliyekuwa akiendesha maombi wakati huo,” msemaji wa polisi alisema.

Msemaji huyo wa polisi, alitaja kuwa katika upekuzi huo, polisi waligundua bunduki aina ya SMG ikiwa na risasi tayari.

"Upekuzi zaidi katika nyumba ya Emodo Vincent ulifichua jarida moja lililokuwa na risasi 29," aliongeza.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Kulingana na msemaji wa polisi, Emodo alikuwa ametoroka ili kukwepa kukamatwa wakati silaha hiyo ilipopatikana.

Walakini, polisi walifanikiwa kumkamata mnamo Oktoba 27, 2024.