Kijana mmoja wa kiume amevutia maoni mengi kwenye mtandao wa X baada ya kudaiwa kuliuza shamba la marehemu baba yake.

Kwa mujibu wa chapisho hilo kwenye kitandazi cha X, Kijana huyo alionekana akiwa ameketi chini kwenye mlango huku wanawake wawili, mmoja akiaminika kuwa mamake akimzomea na kumkaripia kwa fujo.

Inaarifiwa kwamba kijana huyo aliuza shamba la marehemu baba yake kwa Naira za Nigeria milioni 50, sawa na shilingi milioni 3.9 za Kenya na kuzitumia zote katika kucheza Kamari.

Tukio hilo lilinaswa kwenye video iliyosambaa kwenye mtandao wa X (zamani Twitter), ikionyesha wanawake wawili wakimzomea kijana huyo akiwa ameketi, akionekana kuwa na huzuni na mawazo tele.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Kwa nyuma, sauti ya mwanamume inasimulia hali hiyo. Alipoulizwa kilichojiri, alithibitisha kuwa kijana huyo aliuza shamba la babake kwa naira milioni 50 na kutaja kuwa alikusudia kuwekeza pesa hizo kwenye muziki lakini zikaishia kwenye Kamari.

Wakati huohuo, wanawake hao wawili walionekana wakirushiana matusi na kumlaumu mwanawe kwa kitendo chake.

Video hiyo inaposambaa mtandaoni, watu wanaohusika wamefurika sehemu ya maoni ili kutoa maoni yao kuhusu suala hilo.

Tazama baadhi ya maoni hapa chini:

@Ftee95: “Anataka tu pesa maradufu na kununua ardhi bora ?.Nadhani baba yake ni marehemu tayari na yeye sasa ndiye baba wa nyumba sasa kama anaweza kufanya chochote."

@NURUDEENOLUSESI: "Mechi ya wiki iliyopita ilimkosesha tikiti ?️??♂️? atabeba ushindi wa moja kwa moja wa wiki ijayo."