Staa
wa dancehall kutoka Jamaica, Adidja Palmer almaarufu Vybz Kartel aliugua
alipokuwa kwenye akiburudika katika klabu moja ya usiku katika jiji la Kingston
Jumatatu usiku.
Video
za mwimbaji huyo ambaye alitoka gerezani hivi majuzi akisaidiwa na kutoka katika
klabu hiyo zimekuwa zikisambaa kwenye mitandao ya kijamii.
Hili
limezua wasiwasi zaidi kuhusu afya ya mtumbuizaji huyo maarufu hasa kwa kuwa
alitoka gerezani akiwa na dalili kali za ugonjwa wa Graves.
Inasemekana
kwamba Vybz alianza kujisikia vibaya ghafla na watu waliokuwa karibu naye wakaanza
kumpepeta katika jitihada za kumsaidia.
Kisha
msanii huyo alisaidiwa na walinzi wawili, ambao walimshikilia wakati
wakimsafirisha nje kuelekea kwenye gari lililokuwa likisubiri.
Ripoti
kutoka Jamaica zinaeleza kuwa nyota huyo wa dancehall sasa "anaendelea
vizuri" baada ya tukio hilo.
Mnamo Julai 31, 2024, Kartel na washtakiwa wenzake watatu waliachiliwa kutoka gerezani kwa uamuzi uliotolewa na Mahakama ya Rufaa ya Jamaica.
Mashabiki kutoka kote ulimwenguni walisherehekea kuona mwimbaji huyo mwenye umri wa miaka 48 akiungana na familia yake na marafiki baada ya kufungwa kwa takriban miaka 13. Alikuwa gerezani tangu 2011 baada ya kupatikana na hatia ya mauaji ya Clive "Lizard" Williams.
Wakati wa kuachiliwa kwake, alikutana na umati wa wafuasi ambao walimshangilia wakati akitoka gerezani. Hata hivyo, alikuwa amevaa miwani ya jua na kanga ili kuficha uso wake.
Baadaye, picha na video za wazi za msanii huyo ziliibuka zikionyesha jinsi uso na shingo yake ilivyovimba, jambo ambalo lilizua wasiwasi miongoni mwa mashabiki wake.
Iliripotiwa kuwa nyota huyo wa dancehall amekuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa Graves na ugonjwa mbaya wa moyo, ambao ulizingatiwa wakati wa kuachiliwa kwake.
Wakati wa uamuzi huo, iliamuliwa kwamba ugonjwa wa Graves ulitoa hatari ya wazi na ya sasa kwa afya ya Vybz, ambayo inaonekana iliimarisha uamuzi wa kuachiliwa kwake.
Ugonjwa wa Graves, ni hali ya mfumo wa kinga ambayo husababisha mwili kutoa homoni nyingi za tezi, kulingana na Kliniki ya Mayo. Ugonjwa huo unaweza kusababisha ugonjwa wa jicho la tezi, unaonyeshwa na macho makali.
Zaidi ya hayo, Vybz pia anaugua ugonjwa wa moyo.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!