Mwimbaji na mjasiriamali mashuhuri wa Kenya Esther Akoth almaarufu Akothee ameandika barua ndefu ya kihisi kwa mpenzi wake Nelly Oaks huku akimsifu shujaa huyo wake kwa athari kubwa ambayo amekuwa nayo maishani mwake.

Katika barua hiyo aliyoichapisha kwenye akaunti zake za mitandao ya kijamii, mama huyo wa watoto watano alifunguka kuhusu masaibu aliyokuwa akipitia mwaka mmoja uliopita na jinsi mpenzi wake huyo ambaye pia ni meneja wake alivyomsaidia kuyashinda.

Akothee alimtambua Nelly Oaks kama shujaa wake huku akibainisha kuwa alimsaidia sana wakati  ilipohisi kama kwamba ulimwengu wake ulikuwa ukisambaratika.

"Mwaka jana, wakati kama huu, ulimwengu wangu ulikuwa ukiporomoka. Nilikuwa na moyo mzito, roho iliyochoka, mwili uliochoka, moyo uliovunjika, na roho iliyopotea. Nilijawa na maswali mengi—mengi nikijilaumu, na mengine nikiwalaumu wengine. Ndiyo, nilifanya makosa kama binadamu, lakini maamuzi yangu yalikuwa ya haki,” Akothee aliandika.

"Katika kipindi hiki, nilihitaji mfumo dhabiti wa sapoti kuliko hapo awali. Kwa kweli nilihisi kama ulimwengu wangu unazama, kichwa changu tu kikiwa juu ya maji. Kundi la wanawake kwenye TikTok walichukua fursa ya wakati wangu hatari na kuibadilisha kuwa yaliyomo. Waliunda miungano ili kunitukana, kunionea hadi msingi, kunicheka, na kulinganisha huzuni yao na mafanikio yangu dhahiri. Walituma watu wakatukane wazazi na kuidhalilisha familia yangu. Lakini hukunipa kisogo kamwe; ulisimama nami licha ya mashambulizi ya pande zote mbili,” aliongeza.

Mwimbaji huyo alifichua kwamba wakati wa dhiki zake mwaka jana, siku zingine zilikuwa ngumu sana hivi kwamba hakuweza kutoka kitandani.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

"Nilipita siku nyingi bila kutoka nje, nikitazama juu ya dari, na kumuuliza Mungu ikiwa nilimkosea," alisema.

Akothee alibainisha kuwa uhusiano wake na Nelly Oaks ni wa kipekee na akafunguka kuhusu jinsi anavyofurahia muungano wao.

“Ninapenda na kufurahia maisha tunayoshiriki—uchangamfu, mapigano ya hapa na pale, lakini si mengi sana. Watu walikuwa na maoni yao, na walikuwa na uhakika wa 100%. Lakini maoni ni nafuu, na kila mtu ana moja. Mwishowe, ulichagua maoni yako, na ulinichagua mimi., "alisema.

Akothee alibainisha kuwa usaidizi wa Nelly Oaks umekuwa muhimu sana katika maisha yake na alisisitiza mapenzi yake mengi kwa mpenzi wake.

"Barikiwa, mpenzi wangu. Asante sana! @Nellyoaks,” alisema.

Hivi majuzi, mwimbaji huyo mwenye umri wa miaka 43 alidokeza kuhusu kufunga ndoa rasmi na meneja wake katika harusi kubwa ambayo itafanyika hivi karibuni.