Mwimbaji
na mjasiriamali mashuhuri wa Kenya Esther Akoth almaarufu Akothee ameandika
barua ndefu ya kihisi kwa mpenzi wake Nelly Oaks huku akimsifu shujaa huyo wake
kwa athari kubwa ambayo amekuwa nayo maishani mwake.
Katika barua hiyo aliyoichapisha kwenye akaunti zake za mitandao ya kijamii, mama huyo wa watoto watano alifunguka kuhusu masaibu aliyokuwa akipitia mwaka mmoja uliopita na jinsi mpenzi wake huyo ambaye pia ni meneja wake alivyomsaidia kuyashinda.
Akothee
alimtambua Nelly Oaks kama shujaa wake huku akibainisha kuwa alimsaidia sana wakati
ilipohisi kama kwamba ulimwengu wake
ulikuwa ukisambaratika.
"Mwaka
jana, wakati kama huu, ulimwengu wangu ulikuwa ukiporomoka. Nilikuwa na moyo
mzito, roho iliyochoka, mwili uliochoka, moyo uliovunjika, na roho iliyopotea.
Nilijawa na maswali mengi—mengi nikijilaumu, na mengine nikiwalaumu wengine.
Ndiyo, nilifanya makosa kama binadamu, lakini maamuzi yangu yalikuwa ya haki,”
Akothee aliandika.
"Katika
kipindi hiki, nilihitaji mfumo dhabiti wa sapoti kuliko hapo awali. Kwa kweli
nilihisi kama ulimwengu wangu unazama, kichwa changu tu kikiwa juu ya maji.
Kundi la wanawake kwenye TikTok walichukua fursa ya wakati wangu hatari na
kuibadilisha kuwa yaliyomo. Waliunda miungano ili kunitukana, kunionea hadi
msingi, kunicheka, na kulinganisha huzuni yao na mafanikio yangu dhahiri.
Walituma watu wakatukane wazazi na kuidhalilisha familia yangu. Lakini hukunipa
kisogo kamwe; ulisimama nami licha ya mashambulizi ya pande zote mbili,”
aliongeza.
Mwimbaji huyo alifichua kwamba wakati wa dhiki zake mwaka jana, siku zingine zilikuwa ngumu sana hivi kwamba hakuweza kutoka kitandani.
"Nilipita siku nyingi bila kutoka nje, nikitazama juu ya dari, na kumuuliza Mungu ikiwa nilimkosea," alisema.
Akothee
alibainisha kuwa uhusiano wake na Nelly Oaks ni wa kipekee na akafunguka kuhusu
jinsi anavyofurahia muungano wao.
“Ninapenda
na kufurahia maisha tunayoshiriki—uchangamfu, mapigano ya hapa na pale, lakini
si mengi sana. Watu walikuwa na maoni yao, na walikuwa na uhakika wa 100%.
Lakini maoni ni nafuu, na kila mtu ana moja. Mwishowe, ulichagua maoni yako, na
ulinichagua mimi., "alisema.
Akothee
alibainisha kuwa usaidizi wa Nelly Oaks umekuwa muhimu sana katika maisha yake
na alisisitiza mapenzi yake mengi kwa mpenzi wake.
"Barikiwa,
mpenzi wangu. Asante sana! @Nellyoaks,” alisema.
Hivi
majuzi, mwimbaji huyo mwenye umri wa miaka 43 alidokeza kuhusu kufunga ndoa
rasmi na meneja wake katika harusi kubwa ambayo itafanyika hivi karibuni.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!