Rapa mkongwe wa Kenya Paul Julius Nunda almaarufu Jua Cali  anaonekana kuendelea kupata nafuu vizuri baada ya kulazwa hospitalini kutokana na maradhi.

Siku ya Ijumaa, mwimbaji huyo wa nyimbo za genge alionekana kwenye posti za mitandao ya kijamii akiwa na familia na marafiki waliomtembelea hospitalini.

Mwimbaji huyo alichapisha picha za watu mashuhuri kama vile mwanamuziki Wyre, Ala C na mwanamitindo Bashir miongoni mwa wengine waliomtembelea hospitalini. Pia anaonekana akifurahia muda na watoto wake waliokwenda kumtembelea.

"Shukran sana @alacgenge @wyredalovechild kwa kucome thru, shukran," Jua Cali alisema katika moja ya machapisho yake.

Katika post nyingine, alionekana akiwa amewashika binti zake ambao pia walikuwa wamemtembelea wodini.

"Watoto wangu walinijia ili kuniweka sawa," aliandika.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Siku ya Ijumaa, wasimamizi wa Jua Cali kupitia kwa meneja wake Collins Odindo walisema mwimbaji huyo hatacheza katika shoo zijazo kulingana na maagizo ya madaktari.

"Tunasikitika kukujulisha kuwa Jua Cali kwa sasa yuko hospitali chini ya uangalizi." Walisema.

Alisema madaktari wa mwimbaji huyo wamemshauri kukaa kwenye mapumziko ya kitanda na chini ya uangalizi kwa siku mbili hadi tatu zijazo.

Akiongeza, "Tumesikitishwa sana na mabadiliko haya ya matukio haswa kama inakuja kabla ya maonyesho yake ambayo yanatarajiwa wikendi hii."

"Mawazo yetu yako kwa Jua Cali na tunamtakia ahueni ya haraka., Pia tunatoa usaidizi wetu kwa familia, marafiki na mashabiki wakati huu."