
Washukiwa wawili walikamatwa na makachero wa DCI kwa kujifanya kuwa walikuwa wanatoa huduma za ukandaji wa mwili.
Washukiwa hao wawili walikamatwa na makachero wa DCI katika kituo cha Kasarani kwa tuhuma za kuendeleza matangazo katika mitandao ya kijamii kuwa walikuwa wanatoa huduma za kukanda miili ya binadamu.
Washukiwa hao wawili walionyesha ujuzi mkubwa wa kazi yao katika mitandao wakiwa wamejipodoa vizuri na kuwavutia wanaume pamoja na wateja wa kike kwa jumla.
Katika harakati za kuhakikisha kuwa wanawashughulikia wateja wao walikuwa wakiwaibia kila kitu ambacho wateja walikuja nacho pamoja na pesa hivyo kuhatarisha maisha yao.
Watu wengi wamepitai katika hali hiyo ya unyama kutoka kwa washukiwa hao ambao ilisemekana walikuwa wakiendeleza biashara yao kwa muda mrefu bila kukamatwa kabla ya hila zao kugunduliwa na maafisa wa usalama.
Mwathiriwa mmoja aliweza kuripoti tukio hilo kwa maafisa wa polisi katika kituo cha Kasarani ambapo uchuunguzi wa kina kuwahusu ulianzishwa na hatimaye nyama ya hao wangwana ilifichuka.
Washukiwa hawa wamekuwa wakiendeleza shughuli hiyo wakiwa katika mtaa wa Lumumba Drive eneo la Kasarani jijini Nairobi huku wakiwa wamewahujumu raia wengi na hiyo biashara yao ya utapeli.
Katika kisa kimoja kilichosababisha wao kukamatwa ni kuwa waliweza kumwalika mteja mmoja ambapo alimpeleka katika chumba chao cha kutoa huduma za kukanda mwili ambapo walifanikisha shughuli zao kisha kabla ya kutamatisha waliweza kutoa visu vikali na kumwelekezea mteja wao huku wakimtishia maisha tayari kwa kumuua.
Kutokana na hali ya uwoga na kutaka kuokoa maisha yake mteja huyo aliwapa kibali cha kupokea pesa ambapo walimlazimisha kutoa shilingi 280,000 kisha wakachukua vifaa vyake vya thamani hatimaye wakamrusha nje ya chumba.
DCI waliweza kusema na kutangaza kwa kuanzisha uchunguzi wakina tena wa undani zaidi ili kuweza kutambua matapeli wengi ambao wamekuwa na hiyo hulka na tabia ya kuwatapeli watu wengine kwa kutumia njia hizo za hila na ujanja.
Washukiwa hao waliweza kukamatwa na kupelekwa katika kituo cha polisi cha Kamiti na gereza la kamiti ambapo wanazidi kupunga unyunyu huko wakitumia hela hizo alizoiba huku polisi wakiendeleza juhudi za kukamilisha uchunguzi na Kuwafikisha kortini kwa mashitaka.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!