
Mahafali wa chuo kikuu cha Bomet katika kaunti ya Bomet walalamikia ucheleweshaji wa kutoa vyeti vyao.
Mahafali hao walilalamika wakisema kuwa chuo kimechukua muda mwingi kuweza kuwapa vyeti vyao vya masomo licha ya kutamatisha masomo yao kwa muda wa miezi minne iliyopita.
Wanafunzi hao waliofuzu mwaka jana Disemba walisema kuwa walipewa vyeti vya kuhitimu kutoka kwa shule ila hawajapewa cheti cha masomo mbalimbali yaliokuwa wakifanya.
Walisema kuwa matokeo ya kila somo ni muhimu sana kwa maana waajiri huko nje husisitiza kwa kutaka kuona jinsi mwanafunzi alivyokuwa akifauli katika masomo yake.
Kulingana na usemi wa wanafunzi hao walisema kuwa chuo kilikuwa kimekwamilia stakabadhi hizo za masomo kwa misingi kuwa kulikuwepo na hitilafu za kimitambo jambo ambalo lilichochea kukawia kupatikana kwa cheti hicho cha kuonyesha masomo mbalimbali.
Wanafunzi walilalama wakisema kuwa walikuwa wakipoteza nafasi muhimu sana za ajira kutokana na kukosa cheti hicho muhimu ambacho kimekuwa kikiitishwa na waajiri.
Chuo cha Bomet kiliasisiwa kupitia kwa notisi ya sheria nambari 145 mnamo 27 Julai, 2017 kuweza kuhudumu kama chuo mbadala kutoka chuo kikuu cha Moi.
Chuo hicho cha Bomet kimejiweka katika nafasi ya kuhudumu kama chuo ambacho kinajihusisha pakubwa na masomo tekelezi katika nyanja ya Teknohama na Mabadiliko , udhibiti wa mazingira na maendeleo ya ujasiriamali.
Wanafunzi waliweza kusisitiza kwa kusema kuwa chuo kukosa kutoa rekodi nzuri ya hali ya masomo katika chuo hicho hiyo inatishia na kuweka maisha ya masomo yao katika hali ya hatari kwa sababu ya kukosa kupata stakabadhi muhimu za masomo kwa wakati.
Licha ya chuo kusisitiza na kutangaza kuwa kiko imara kwa kutoa mafunzo tekelezi katika nyanja mbalimbali na kwa kudhihirisha kuwa mambo haya yanafanikishiwa ni lazima chuo kiweze kuweka misingi imara tena dhabiti kwa kuhakikisha kuwa wanafunzi hawapati wakati mgumu wakati wa na baada ya kutamatisha masomo yao.
Huwa ni furaha kwa mzazi pamoja na mwanafunzi kuhitimisha masomo yake kisha kufanikiwa kwa kupata ajira hiyo huwa ni jambo la kufurahia na huleta shangwe kwa jamii.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!