Gari  Toyota  Prado

Mfanyabiasha mmoja anayedaiwa kuendeleza biashara ya uuzaji wa magari akabiliwa  na tuhuma  za kutolipa ushuru.

Mfanyabiashara  huyo mwanzoni aliyeripotiwa  kwenye asasi za  uongozi na  akalazimika kusitisha biashara  hiyo imebainika kuwa tena ameifufua biashara hiyo  na kuipa jina  jipya.

 Kulingana na baadhi ya wateja wa huyo mfanyabiashara  inasemekana kuwa alikuwa akiwaahidi wateja wake  kwa  kuwauzia magari huku baada ya  malipo kufanyika  kuna  muda  mwingi wa kuwasilisha gari hilo kwa mteja  husika.

Ilisemekana kuwa mfanyabiashara huyo alikuwa na  mazoea ya kuchelewesha uwasilishaji wa  magari kwa wateja wake sababu kuu ikiwa ni kuwa mfanyabiashara huyo wa  magari alikuwa anatumia njia  ya mkato kupitisha magari katika bandari ya Mombasa kwa kutolipa ushuru ifaavyo.

Mshukiwa huyo ambaye ana biashara ya umiliki wa magari kwa  jina House of  Cars iliyo katika vichorochoro vya Jobavu  Nairobi mwanzoni aliwahi kuhusishwa na kampuni ya magari ya Kheng Kheng ambayo inadiwa kuwa  ilibadilisha jina  ila  huduma  zake  zilisalia zilezile.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Katika msururru wa  matukio ya arafa mteja mmoja alimshutumu mfanyabiashra  huyo kwa kuweka kiasi cha shilingi milioni  3.95  Agosti Mwaka jana 2024  kwa ajili ya  kununua na kumpokeza gari  aina ya Toyota Prado ila  hakuwasilisha gari kwa mteja wake miezi kadhaa baadaye.

Alisema kuwa angemrudishia mteja wake pesa  Januari mwaka huu 2025 ila pesa hizo kufikia  sasa hazijarudishwa. jambo lililosababisha  mlalamishi kuripoti tukio hilo katika kituo cha polisi cha Muthaiga.

Hata baada ya hapo hakuna lolote la ziada  ambalo limefaaanyika kufanikisha upatikanaji wa haki upande  wake licha ya kuendelea kulipa mkopo wa benki kutoka kwa Benki ya NCBA  kulipa hela hizo.

Kuna  madai kuwa mfanyabiashara  huyu huwa  na ukuruba  na  ushirikiano wa  karibu sana na maafisa  wa bandarini Mombasa ambao humsaidia kuweza  kukwepa ulipaji wa ushuru kwa KRA Pamoja na kusitisha huduma zote  zinazohusiana na uagizaji wa magari kwa wateja wake baada ya wateja kulipa.

Hata hivyo umma  umeombwa kuwa  macho na makini wanapofanya  ushirikiano wa kibiashara na mfanyabiashara  huyo kwa  ajili ya  usalama  wao.