Kauli ya Mbunge Ndindi Nyoro kuhusu uchumi wa Kenya Aprili, 15 2025

Mbunge wa Kiharu Ndindi Nyoro huyo ambaye aliondolewa kama mwenyekiti wa kamati ya bunge ya bajeti alikosoa hatua ya serikali ya rais William Ruto kwa kuongeza ushuru mwaka 2022 akisema kwamba ilidhoofisha uchumi wa taifa.

Alisema kwamba kupandishia wananchi  na wawekezaji ushuru hakuongezi pato kwa serikali bali hupunguza kiwango cha ushuru unaokusanywa kutokana na kupungua kwa shughuli za kiuchumi.