Mkutano wa pamoja kuhusu usalama wa uchimbaji wa madini

Waziri wa usalama  Kipchumba Murkomen alishirika katika mkutano wa usalama wa uchimbaji wa madini.Ni mkutano uliofanyika tarehe  16 Aprili, 2025 jijini Nairobi.

'' Idara ya uchimbaji madini ni muhimu tena huchangia pakubwa katika  ukuuzi wa uchumi wa nchi ila  kuwezesha asasi za kulinda usalama kutulia pasi kuangazia usalama wa hali hiyo ambapo ni hatari.

Makuuzi ya nyanja hiyo yamenyamaa na kuvuvia kutokana na uchimbaji wa madini ambao si halali na ambao unasitahili kudhibitiwa  na  kuwekwa  katika shajara ya serikali'' Murkomen alieleza.

Kando na kupoteza mapato  pamoja na kupata kiwango cha chini cha wawekezaji ambao ni waaminifu, uchimbaji wa madini ambao si halali pia  huweza  kuharibu mazingra, kuleta vita kung'ang'aniwa kwa raslimali, hali ya afya kuwa  mbaya, ajira kwa watoto wadogo na usalama kuhusu wananchi.

Kulingana na mwelekeo wa huduma ya polisi  kwa taifa pamoja na kampeni endelavu ya jukwaa la usalama ukanda wa Pwani hayo ni baadhi ya masuala ambayo yalikwa yanaikumba wizara na  idara ya  uchimbaji madini nchini.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Kutokana na hayo wizara ya usalama iliazimia  kufanya mabadiliko katika idara  ya madini kwa  kuwaongezea maafisa  wa usalama ambao watakuwa  na jukumu la kutahimini jamii kwa  kuangazia ni wapi zoezi la uchimbaji madini litakuwa likiendelea  pamoja na kuhakikisha kuwa shughuli hiyo inafanikishwa kwa usalama  kwa  kuwepo kwa usalama wa taifa.

Waziri Murkomen alikuwa ameandaa mkutano huo uliowaleta  pamoja washikadaau wote katika wizara zote mbili wizara ya usalama na wizara  ya uchimbaji wa madini  iliku boresha shughuli  hiyo muhimu.

Maafisa waliohudhuria mkutano huo wa pamoja ni waziri wa uchimbaji madini na  uchumi wa majini   waziri Hassan Joho, katibu mkuu katika idara ya uchimbji wa  madini Harry Kimtai, inspekta mkuu wa polisi   Douglas Kanja, Naibu afisa mkuu wa polisi  Eliud Lagat naibu insipekta mkuu wa  polisi Gilbert Masengeli, mkurugenzi mkuu wa DCI Mohamed Amin miongoni mwa maafisa wengine wa usalama.

Mkutano huo ulipania kutoa suluhisho kuhusu uchimbaji wa madini na kuhakikisha kuwa  iwapo shughuli hio inatekelezwa inaafikia viwango hitajika vya kisheria.