
Huduma ya Polisi kwa umma ilitoa taarifa rasmi kuhusiana na operesheni ya Polisi inayoendelea Haiti.
Huduma hiyo ya taifa ya polisi iliweza kusema kuwa iliweza kuona habari zilizokuwa zikisambaa katika gazeti la Daily Nation la tarehe 15, Aprili,2025 lililokuwa likitilia shaka ufaafu wa maafisa wetu katika operesheni ya kijeshi nchini Haiti.
Huduma hiyo ilisema kuwa ilipinga vikali na kulaani habari hizo ikizitaja kama zisizo za kweli na ambazo zimekosa uzalendo wa taifa.
Huduma hiyo ya polisi iliweza kusema kuwa utoaji wa maafisa hao wa polisi kuenda katika taifa la Haiti kwa ajili ya Operesheni ni kutokana na maafikiano ya umoja wa mataifa kuhusu kusuluhisha masuala na vita na upatikanaji wa amani katika nambari 2699 ya mwaka 2023.
Kutokana na maafikiano hayo ndipo maamuzi ya Kenya kuweza kutoa usaidizi kwa taifa la Haiti ili kuweza kuhakikisha,usalama unaafikiwa kwa taifa hilo la Haiti ambalo limekumbwa na maasi kutoka kwa magaidi.
Kulingana na ripoti ya Huduma ya polisi ilisema kuwa polisi walikuwa wamepewa kazi mafunzo ya kutosha kuhusu jinsi ya kutumia mambo kadhaa yakiwemo utumizi wa Bunduki maalum za vita.
Vilevile walikuwa wamejifunza jinsi ya kudhibiti umma kwa kiwango cha juu, sheria za kimataifa na sheria na haki za binadamu, polisi waliweza kujifunza jinsi ya kulinda amani na vilevile kujifunza jinsi ya kuzungumza Lugha ya Kifaransa.
Huduma ya Polisi iliweza kusema kuwa kwa kuzingatia mafunzo hayo yaliweza kuwapa nafasi ya kuweza kuendeleza huduma zao za operesheni bila matata yoyote.
Maafisa waliweza kupewa magari ya spesheli ya kivita kama vile MRAPS, balistiki Helimeti, nguo za karandinga na jinsi ya pamoja na vifaa ambavyo vinawasaidia kuweza kuhakikisha kuwa kila kitu kiko shwari ni ajili ya kupambana na operesheni hiyo.
Kulinganna na ripoti ya usalama wa kimataifa ambayo Kenya imekuwa ikishiriki ilikuwa wazi kuwa wangefanikisha operesheni hiyo kwa kuhakikisha kuwa wanafaniksha misheni hiyo maaluum bila kutatizika.
Kutokana na historia pana tena yenye ufanisi mkubwa ambayo Polisi Wa Kenya wameshiriki ni kuhakikisha kuwa kila kitu kinafaulu na kwa kufaulisha shugul hiyo ya usalama Haiti hiyo ni kuipa sifa taifa la Kenya Pamoja na umoja wa kimataifa.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!