
Waziri wa mazingira na misitu Deborah Barasa alihudhuria kikao cha pamoja na ubalozi wa ufaranja ili kujadili masuala muhimu ya mazingira jijini Nairobi.
'' Nimeshiriki mazungumzo na wajumbe katika mkutano wa kimataifa na balozi wa Ufaranja Agnes Pannier Runacher pamoja na waziri wa masuala ya maisha ya vimelea vya ardhini pamoja na maisha ya mazingira yanayowazunguka wanyama hao.
Vilevile kulikuwepo na mabadiliko ya misimu, misitu,na wanyama wa majini na uvuvi, ambapo mazungumzo yalijikita pakubwa katika kuimarisha mabadiliko ya tabianchi duniani kuongeza na kuzamia katika mabadiliko ya tabianchi duniani'' Debora alieleza.
Huo mkutano ulijiri wakati ambapo kunatarajiwa kuwa na mkutano wa kimataifa kuhusu mipango na mikakati ya kuwa na mazingira mema alimaarufu UNFCCC COP30 mji wa Belem Brazil kwa kuhakikisha kuwa tunakuwa na usawa kwa kuhakikisha kuwa tunakuwa na mazingira mazuri pamoja na tabianchi ambayo ni sawa kote Afrika.
Ushirikiano wa taifa la Kenya na Ufaransa uliafikia ufanisi mkubwa katika kuhakikisha kuwa kunajengeka mifumo imara tena dhabiti kuhusu mwendelezo kuhusu masuala ya tabianchi,ambapo lengo kuu ni kuhakikisha kuwa kunakuwa na kujengeka kwa mazingira ambayo ni mwanzo wa kuimarisha uhusiano mwema wa kimataifa.
Katika Mkutano huo kulikuwepo na balozi kutoka taifa la Ufaransa Kenya Arnaud Suquet, Katibu mkuu katika masuala ya mazingira , Bwana Gitonga Mugambi wa Misitu,Betsy Njagi wa uchumi wa majini miongoni mwa viongozi wengine wengi.
Masuala ya mazingira hasa katika suala la Tabianchi limekuwa likizungumziwa sana kwa muda mrefu huku mataifa yote yakiwa na rai kuwa angalau kuwe na ushirikiano wa karibu ili kuepuka kuharibu mazingira haya ya tabianchi.
Taifa la kenya limekuwa likishniriki katika makongamano kadhaa kuhusiana na masuala ya tabianchni ili kuhakikisha kuwa kuna ufanisi wa kipekee kwa kujenga na kuwa na mazingira ambayo ni salama kwa mataifa yote.
Mataifa ya Afrika yamekuwa yakitoa wito kwa mataifa ya ulaya kuweza kufidia au kuongza kiwango cha kutoa pesa kwa ushikiano wa kidunia wa kulinda mazingira ya tabianchi kwa kusema kuwa mara nyingi yamekuwa yakiharibu mazingira kwa kutoa gesi chafu kwa wingi.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!