Bodaboda na kinamama eneobunge la Kiambaa

Serikali ilianzisha mpango  wa kutoa michango kwa  wanabodaboda na akina mama  eneobunge  la Kiambaa

Ni shuguhuli iliyofanyika katika  shule ya upili ya Karuri eneobunge la Kiamba kaunti ya Kiambu.

Ni hafla ambayo ilihudhuriwa  na viongozi wakuu serikalini wakiongozwa na Naibu wa rais Profesa Abraham Kithure Kindiki, kiongozi wa walio wengi  bungeni Kimani Ichungw'ah, mbunge  wa Kapseret Oscar Sudi miongoni mwa  viongozi wengine.

 Katika hafla hiyo ambayo ilikuwa na mbwembwe pamoja  na wananchi waliofurika kuweza kuhudhuria  shughuli hiyo viongozi mbalimbali waliweza kutoa hotuba zao kuweza kuisifia serikali na kuwarai wananchi waweze kuiunga mkono  serikali kikamilifu.

 Reuben Kiborek mbunge wa Mogotio aliweza kusema kuwa wananchi walistahiki kuwa watulivu huku serikali ikihakikisha kuwa inatimiza kila ahadi iliyoahidi ilipoingia mamlakani.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

''Viongozi wengi wamekuwepo katika uongozi wa  taifa wakati ambapo kulikuwa na viongozi wengine wakawa wanakumbana na chngamoto  mlisema kuwa tuipe serikali muda ili iweze kutekeleza ahadi zake na wakati ambapo kiongozi wetu amechukua mamlaka watu wanaanza kusema ni lazima aende aaaah je  hiyo  ni haki kweli?''Mbunge Reuben Kiborek alisema.

 Kwa upande  mwingine Mbunge wa Kapsaret  Sudi aliweza kusema kuwa haiwezekani kutafuta au kufanya kazi kwa bidii ili kupata jambo kisha baadaye uwachiliee  tena urudi katika viwango  vya kuanza kutafuta tena kwa kwanza kwa  hatua moja.

'' Haiwezekani kwa mtu kuweza kutafuta jambo kwa muda mrefu kisha ukishapata  unaachilia tena uanze kutafuta upya  ni kama  tu utafute chakula kwa kusumbukana kisha ukipata mlo tena unapiga teke  unarudi tena kuanza kutafuta la hasha ha iwezekani.'' Oscar Sudi alisema.

kwa upande wake Naibu wa Rais Kithure  Kindiki aliweza kusema kuwa  kama tu viongozi  waliotangulia  na  kufanikisha  maendeleo ya kuisukuma nchi mbele  na kuendelea kupiga  hatua aliwahakikishia wakazi wa Eneobunge  la  Kiambaa  kuwa nao walikuwa  katika harakati ya kuhakikisha kuwa taifa linasonga mbele kimaendeleo.

Tangu  serikali ya Kenya Kwanza ilipochukua hatamu za  uongozi hio ndio hafla ya  kwanza ya kuweza kuandaliwa ambapo ilikuwa ikipigia debe  mfumo wa  kuhakikisha  kuwa inapata kumuinua mtu wa kiwango cha chini.

Katika hafla hiyo  Kindiki alitoa mchango  wa shilingi milioni tatu kwa niaba ya rais  huku yeye akitoa milioni mbili  vilevile mbunge Oscar Sudi alitioa kitita cha shilingi milioni mbili, Kimani ichungwa  akitoa mchango wa  shilingi milioni moja ilihali  wabunge wengine wakitoa  michngo ya  shilingoi laki moja .