Kiongozi wa chama cha DAP Kenya

Kiongozi wa chama cha DAP Kenya Eugene  Wamalwa alisema kuwa wanafunzi walikuwa wakiwasilisha ujumbe muhimu kwa Wakenya kupitia kwa mchezo wa  kuigiza.

Wamalwa alikuwa  akirejelea  matukio yaliofanyika mnamo Alihamisi 10 Aprili, 2025 katika Kaunti ya Nakuru ambapo wanafunzi wa shule  ya upili ya wasichana  ya  Butere walizuiwa na maafisa wa usalama kuweza kuigiza  mchezo  wao wa  Echoes  of War.

Alikuwa akizungumza  katika kituo cha Runinga cha NTV asubuhi wakati alipoulizwa  aelezee msimamo wake kuhusu tukio hilo lililojiri katika Kaunti ya Nakuru.

 Wamalwa alisema kuwa Maudhui ambayo yalikuwa yamebebwa  katika mchezo huo yalikuwa ni masuala ambayo yalifaa  kusikilizwa  na  kutazamwa na wakenya  pamoja na wananchi ili waweze kusikiliza  na kujitathimini ipasavyo. 

Kulingana na matamshi ya  mheshimiwa Wamalwa alisema kuwa serikali ilikuwa imesusia kadamnasi na peupe kuwasikiliza  viongozi kutoka matabaka  mbalimbli wakiowemo viongozi wa dini kuhusu hali halisi ya matibabu na  hali ya uchumi nchini.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

'' Mwanzo kabisa wacha  nianze kwa kuwapongeza na kuwashukuru wanafunzi kutoka  shule ya upili ya  Butere  kwa  kuonyesha ujasiri wa  kipekee katika harakati na pilikapilika  za kuhakikisa kuwa wanafahamisha  umma kuhusu ukweli  ambao unatusonga kama taifa.

Wanafunzi walikuwa na ujumbe  mwema  wa  kumwarifu rais kuwa alikuwa uchi kutokana na  masuala ambayo yalikuwa yanafanyika nchini kuhusu  mambo ya Ukosefu  wa ajira, Hali ngumu ya  maisha ,utekaji nyara, utozaji wa ushuru wa  juu kwa  wakenya miongoni mwa masuala ambayo yallikuwa  yakiwaathirii wakenya  kama suala la  Bima ya matibabu ya SHA.

Wamalwa  alisema kuwa huo ujumbe  ulikuwa umebeba mambo ambayo rais  angesikiliza  na kutazama  angelikuwa na wakati mwema  wa  kuyashughulikia  kwa  sababu washauri wa kike  pamoja  na wale watu ambao walikuwa karibu na yeye walikuwwa wamemwangusha kwa  kutomshauri na  kumweleza ukweli wa Mambao jin si inavyo faa'' Wamalwa alisema.

 Katika usemi wake  Eugene  alisema  kuwa katika enzi zake akiwa shuleni alikuwa mwana drama na aliweza kuwasilisha  michezo ya kuigiza  mbele ya rais   Moi moja kwa  moja  wapo  ikiwemo ya kupinga madhila na  dhuluma Moi alikuwa akizielekeza  kwa  wananchi  enzi zake.

 Vilevile Eugine  Alishangaa ni kwa nini mama wa Taifa Bi Rachael Ruto alisalia kimya  kuhusu hilo  suala la  shule ya B utere ilihali ilikuwa shule  yake  ya  zamani.