Afisi ya insipekta mkuu wa polisi ilitoa  taarifa  kamili kuhusiana  na matukio ya Drama katika  Kaunti ya Nakuru kuhusiana na Shule ya Upili ya wasichana ya Butere.

''Huduma ya polisi ya taifa ambayo inatambulikana katika kifungu nambari 244 cha katiba  ni moja  kati ya  hitaji muhimu  la  usalama ni nguzo muhimu ya usalama ambayo ina jukumu  la kulinda na kudhibiti  mali na maisha ya  wananchi bila  kuvunja  haki za wananchi.

Huduma hii ya polisi ina jukumu kuu la kuhakikisha kuwa inalinda huduma zote za  michezo katika  mashindano ya drama kwa shule  za  upili na vyuo  vikuu  katika kiwango cha kitaifa kwa kuhakikisha kuwa shughuli iyo inafanikishwa bila vizingiti vyovyote.

Mnamo siku ya Alihamisi 10, Aprili, 2025 tulipokea habari za kijasusi za   kuaminika  kuwa kulikuwa na watu  ambao walikuwa wanapanga kusambaratisha  mashindano hayo ya sherehe  na kama huduma ambayo ina wajibu  wa kuhakikisha kuwa usalama unakuwepo tuko imara  na mstari wa mbele  kuweka mikakati ya usalama ili kuzuia mpango huo.

Hata  hivyo kuna madai kulikuwa  na matukio ya matumizi mabaya ya mamlaka kutoka kwa  baadhi ya  maafisa wetu wa  usalama waliopelekwa huko Nakuru kwa ajili ya kuhakikisha kuwa  usalama una dumishwa ipasvyo.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Inspekta mkuu wa polisi  aliweza  kuamurisha uchunguzi wa  haraka wa madai hayo kwa  maafisa  wa polisi ambao kwa namna moja au  nyingine  waliweza  kuhusika katika mienendo mibaya  ili  hatua za  kisheria  ziweze  kuchukuliwa.

Afisi ya inispekta  wa polisi  iliweza kutangaza kwa kusema kuwa  vitengo maalum  ambavyo vinashughulikia masuala  ya  huduma za  polisi kama   IPOA pamoja na kikosi cha kuchunguza  masuala  ya ndani kiweze  kufanya uchungunzi wa kina  kuhusu maadai hayo na  kutoa ripoti chini ya  siku 21 zijazo. 

Huduma  ya  polisi inajitoa kwa kuhakikisha kuwa  inatoa huduma za usalama kwa uwazi , uwaminifu na kwa kuzingatia katiba bila kuwa  na muegemeo wowote wa kisiasa  bali kwa  kuzingatia sheria  na kutii na vilevile  inaruhusu  uhuru wa kunjieleza kwa kila mmoja pamoja na kutangamana   bila  vizuizi'' mwisho wa nukuu ya barua.