caption

Manaibu  Gavana wasisitiza  kutengewa  bajeti  yao kando ili kuendeleza kamati  mbalimbali katika Kaunti.

Manaibu wa magavana walielendeleza wito wa  kutaka kupewa bajeti  yao katika masuala  ya uongozi.

Walizungumuzia swala hilo  kwenye bunge la Seneti kuhusu masuala  ya ugatuzi wakiongozwa na mwenyekiti wao Reuben Kamuri.

 Manaibu  magavana  hao waliweza kusema kuwa wana ujuzi na uwezo wa kuweza  kutekeleza majukumu  mengine  ya  uongozi katika  serikali za kaunti na kuimarisha uongozi mwema.

Waliweza kusema kuwa  kwa mara nyingi wamekuwa wakisalia kupangwa  na magavana wao bila  kupewa  majukumu maalum ya kufanya  kazi.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Waliweza kusema kuwa wangependa Katiba iweze kubadilishwa ili kuwe na bajeti yao maalum  Pamoja na kazi zao ambazo zinatambulikana  kikatiba.

 Walisema kuwa  kwa mara nyingi magavana wamekuwa wakiwatumia kutafuta kura  baaada ya hapo wanawatelekeza  na  kuwawacha katika hali  ngumu  bila wao kujua  hatima  yao ya uongozi.

 Usemi wa  uliweza  kuungwa  mkono na baadhi ya maseneta  kama  Mpuri  Aburi wa Meru waliosemkuwa  kwa  hakika manaibau magavana wamekuwa wakipitia  hali ngumu  katika wakati wao wa uongozi kwa kukosa kazi mwafaka na  inayotambulikana  kisheria.

‘’Ni wazi kuhusu kile mbacho   manaibu wa magavana wanastahili kuwa wakifanya lakini  ni  jambo la kusikitisha kuona  magavana  hao wanafanya kazi katika huruma ya Magavana jambo ambalo ni  la kusikitisha  sana inasitahili sheria zibadilishwe ili tuwe  na kazi  maalumu na bajeti  maalum  ya  kutekeleza  baadhi ya  miradi  mbalimbali  katika  serikali za  kaunti’’. Ruben Kamuri mwenyekiti wa kamati ya bunge  kuhusu ugatuzi alisema.

‘’ Ninaunga mkono pendekezo hilo la manaibu magavana  kupewa bajeti yao ili waweze  pia  kuendeleza baadhi  ya sera za  maendeleo katika uongozi wa Kaunti mwanzo hawa  viongozi wana ujuzi na tajiriba  pana kuhusu uongozi’’ Mpuri Aburi alisema

 Kwa mara si moja kumeshuhudiwa  mizozo na  mwingiliano wa masuala ya uongozi kati ya magavana na manaibu wao kuhusu uongozi jambo ambalo huisha kusababisha kukuwa  na miswada ya kung’atua magavana uongozini jambo ambalo huleta vita vya kimaslahi.