Naibu  rais Kithure  Kindiki amekutana na mawaziri mbalimbali kujadili ufanikishaji wa  maendeleo ya serikali.

Alikutana na mawaziri hao katika makao makuu yake ya   Karen Nairobi  ili kujadili  ufanikishaji wa  maendeleo  ya  serikali  mnamo  Aprili 11,2025.

'' Kamati za  mabaraza  huweza kurahihisha  na kufanikisha utoaji wa  huduma  katika kamati za   mabaraza kwa  kuhakikisha kuwa ajenda,sera, miradi na maendeleo  ya serikali inawafikishwa  kwa ajili  ya  wananchi kwa  haraka'' Kindiki aliandika katika ukurasa wake wa X.

.Alihitimisha mkutano huo kwa kufanya mazungumzo mapanna kwa kuweza  kufanya kikao maalum na wizara  ya fedha barabara, wizara ya ardhi nyumba  na makao  ambapo masuala mengi yanayohusiana na kuimarisha uchumi , kuendeleza kupata  masoko mbalimbali ya kifedha na  vilevile kuendeleza  uongozi  bora ni baadhi ya masuala ambayo yalijadiliwa  kwa upana zaidi katika kiao hicho.

Profesa Kithure  Kindiki alichukua  jukumu hilo ili kuweza  kuongoza baraza la mawaziri kama jukumu lake kuu la  kikatiba  ambalo anastahili kulitekekeza kisheria.

 Mawaziri mbalimbali  kutoka  katika wizara zao huweza  kuleta  ripoti maalum ya  jinsi wizara na idara zao zinavyopiga  hatua kimaendeleo ikiwemo changamoto ambazo zinapitia na halikadhalika  suala la ukaguzi wa  maendeleo na hatua  chanya pia  huweza  kuangaziwa  ipasavyo katika  kikao hicho cha mawaziri.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Baada ya masuala  hayo  yote  kujadiliwa na kila  wizara kutoa maelezo  muhimu ya kile  ambacho kinahitajika kuwa kinafanyika na  hatimaye  ripoti  ya mwisho kuandikwa ambapo Naibu wa rais  huweza  kumpekelekea rais ambaye huisoma na kueza kutoa maoni yake  kuhusu  majadiliano na hali nzima  ya  baraza.

Katika  kikao cha tarehe 11 Aprili, 2025 mawaziri waliohudhuria ni Alice Wahome wa Ardhi nyumba  na makao,John Mbadi Waziri wa Fedha,Davis Chirchir wa barabara,James opiyo Wandayi waziri wa Kawi,waziri wa  mazingira Deborah Barasa,waziri wa utali Rebecca Miano,Mwanasheria mkuu  Dorcas Oduor,na  katibu wa baraza  la mawziri Mercy Wanjau pia  alikuwepo  katika mkutano huo. hii ni kuashiria kuwa mawaziri hawa wanajizatiti kwa kila mmoja kuhakikisha kuwa wanatekeleza wajibu wao wa kikatiba.