Mkutano wa wizara ya afya na KMPDU

Waziri wa afya Adeni duale alifanya mkutano na muungano wa makitari nchini KMPDU

Ni mkutano ambao ulifanyika mnamo  tarehe 10 Aprili 2025 katika  jumba la  afya jijini Nairobi.Muungno huo wa madaktari uliweza kuwakilishwa na katibu mkuu wa muungano  huo  Daktari Davji Bhimji Atellah na mwenyekiti  Daktari Abidan Mwachi ana viongozi wengine wa ngazi za juu katika  muungano huo.

Wazrir Duale aliweza kuandamana  na katibu wake wa kudumu Mary Muthoni  ambapo kupitia  kwa wizara hiyo ya afya ilijitolea kuhakikisha kuwa inajenga ukuruba  na kufanikisha mipango miema na muungano wa madaktari.

Wizara iliweza  kuhakikisha kuwa na kusema kuwa ilikuwa imejitolea kwa kuwapongeza matabibu wato kwa kuhakikisha kuwa walikuwa wanafanya kazi kwa kujitolea na kuweza kuleta uhusiano mzuri.

Wizara iliweza kuwapongeza madaktari kwa kuwa mstari wa mbele kwa kuwashughulikia wagonjwa kwa kuwapa matibabu kwa usawa na kwa moyo wa kujitolea.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

 Hata hivyo wizara iliweza kusema kuwa kutokana na juhudi na bidii ambazo madaktari wamekuwa wakifanya wiza ra ya afya  ilikuwa na mpango mwema wa kuhakikisha kuwa inashughulikia matakwa na maslahi yao kwa uzuri kwa kuhakikisha kuwa inaimarisha mifumo ya afya kwa wote  alimaaruufu taifa care.

Wizara  kupitia kwa Duale ilisema kuwa ilikuwa inashirikiana  na washikadau mbalimbali ili kuhakikisha kuwa inawapa madaktari maslahi ambayo yanafaa na vilevile kuweza  kuzungumza ili kupata  suluhisho ya kudumu kutokana na malimbikizi ya mishahara na mikataba  mabalimbali.

Duale pia aliweza kusema kuwa kama wizara walikuwa katika hali ya kuhakikisha kuwa wanajitolea ili kuweza kufanikisha na kutekeleza mikataba yote ambayo imekuwepo kwa muda mwingi  na ambayo haijatekelezwa.

Duale alishukuru sana muungano wa madaktari pamoja na viongozi wao kwa  kuwa mstari wa mbele na kuonyesha ari  ya kushiriki  katika midahalo ya upatanishi ambayo inalenga kuhakikisha kuwa  pande zote zinatimiza malengo husika kwa uzuri.

Duale alisema kuwa kutokana na hio mipango mipana kwa  ushirikiano na madaktari  hawa kutakuwa na ufanisi mkubwa  katika wizara ya afya na kukuza umoja na kufanikisha mpango wa afya kwa wote alimaarufu UHC kote nchini.