Seneta wa zamani wa Kakamega na mwandishi wa tamthilia tatanishi ya Echoes of War alilala katika kituo cha polisi cha Eldamaravine.
Akizungumza na kituo cha Runinga cha Citizen mnamo tarehe 10 Aprili kupitia kwa njia ya simu na mtangazaji Rashid Abdala alielezea wananchi kuhusu hali yake ilivyo.
'' Jana nilikuona ukiwa umezuiliwa ili kutoweza kuwasalimia wanafunzi wako na kuwajulia hali huku ukiwa katika pilikapilika za kuhakikisha kuwa unajianda kwa hafla ya siku iliyofuata, sijui kwa sasa uko wapi na ulilala wapi? Rashid Abdala alimuuliza.
Kwa sasa niko katika kitu cha polisi cha EldamaRavine hapa ndiko nilikolala kwa sasa hivi bado nimeshikwa niko katika kituo cha polisi,polisi wamejaa huko nje na ilihali wamekatata kuniambaia makosa yangu ni gani?
Ninakashifu hicho kitendo vikali kwa maana ni kitendo ambacho kinalenga kuwaadhalilisha na ninalaani kitendo cha kuweza kuwaondoa na kuwanyima watoto wetu uhuru wa kujieleza na kuweza kuimarisha vipaji vyetu kwa kutumia talanta.
Nimekuwa nikiuliza makosa yangu ni gani kuhussu kushikwa huku kisha ninaambiwa kuwa ni amri kutoka juu kwa hivyo nigependa kumrai rais pamoja na uongozi wa serikali kuu kwa jumla ningependa kumwambia rais kuwa vita vyetu kama wanasiasa visitumike kuwaelekezea watoto pia.
Rais ni vipi unakanya mchezo huo usichezwe na ilihali haujauona tena ningependa kusema kuwa mchezo huu ulianza kupata ushindi katika viwando vya maeneo bunge na kuweza kushinda katika ngazi ya mkoa na kupata alama 90 kuashiria kuwa ni mchezo wa kuigizwa ambao una tija sana kwa jamii.
Ila kwa upande wangu ningependa kusema kuwa tuweke kando siasa na kuweza kuhimiza umoja na utangamano bila kuwajumuisha watoto wadogo ni haki yao kushiriki katika michezo hii ya kuigizwa'' Malala alisema.
Alipoulizwa kuhusu kile ambacho sasa alikuwa ameandikisha kortini kutokana na kukamatwa kwake alisema kuwa hapakukuwa na andikisho lolote la makosa yake ila akasema kuwa mawakili wake wakiongozwa na wakili Ken Echesa walikuwa wakifanya kila juhudi kwa ushirikiano na afisi ya mkurugenzi ya mashitaka ya umma ODPP ili kuweza kutegua kitedawili hicho.
Wanafunzi wa Butere waliweza kufika katika jukwaa kisha wakaaimba wimbo wa taifa na hatimaye wakaondoka kulingna na video na sauti zilizonaswa.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!