Waziri wa usalama wa ndani Kipchumba Murkomen

Waziri wa usalama wa ndani Kipchumba Murkomen aliendeleza  kampeni  yake ya usalama katika eneo la Pwani ya Kenya. 

 Ni kampeni ambayo  aliipa jina la  Jukwaa la usalama maeneo ya pwani ya  Kenya ambapo ililenga kutoa usalama kwa wakaazi wa eneo hilo na kuondoa makwekwe na vizingiti katika maeneo hayo.

Katika shughuli ya kutupilia  mbali zoezi la upigaji msasa wa wananchi kwa ajili ya kupata vitambulisho pia  lilijadiliwa katika msururu wa  kampeni ya usalama katikla eneo hilo.

Vilevile aliweza kuzungumzia suala la kupata vitambulisho bila kuhitaji kutuma maombni zaidi  na kuweza  kusubiri kwa muda kama awali  huku akisema kuwa hatua hiyo kwa sasa serikali ilikuwawa  imechukua   hatua  madhubuti kwa kuhakikisha kuwa wananchi wote wanapokea vitambulisho hivho bila  kutatizika akisema kuwa ilikuwa huduma ambayo ilikuwa  ikitolewa kwa  wananchi wote  bila kuzingatia ubaguzi wowote.

Waziri Murkomen pia  aliweza kukagua zoezi hilo katika eneo bunge la Mokowe   ambapo  shughuli  ya watu kujisajili kwa ajili ya kupata vitambulisho lilikuwa likiendelea katika  kaunti hiyo ya Lamu.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

''Tutasikiliza na  kuwashirikisha maafisa  wa  usalama katika vitengo vyote  ili kuhakikisha kuwa tunawasikiliza  washikadau  wote  wakiwemo wananchi kuhusiana na  matukio ya usalama.

 Vilevilee huduma za usalama kwa wananchi pia zitaaweza kutolewa ili  wananchi waweze  kufaulisha mipango yao kwa kupata huduma zote  za serikali kutoka kwa serikali bila  ubaguzi wala upendeleo wowote '' Waziri Murkomen aliweza kufafanua,.

Itakumbukwa  wazi kuwa waziri Murkomeni  amekuwa  katika pilikapilika za kuendeleza  shughuli za  usalama katika sehemu zote  za  taifa ikiwemo na kujihakikisha kuwa anahamasisha umma ni kwa ajili ya kuwaeleza ili waweze kujisajili  na kupata vitambulisho vya kitaifa.

Mwezi  jana  aliendeleza zoezi hili katika kaunti ya Nakuru  huku akiwahiimiza  watu kuhakikisgha kuwa wanajisajili ili kupata huduma  hiyo muhnimu ya kitambulisho.

Katika  Kaunti ya Lamu aliweza  kuandamana na viongozi kama Gavana Issa Timamy  seneta Joseph Gichuki, mbunge Obo Ruweida Lamu mashariki, Stanley Muthama wa Lamu magharibi na naibu inspekta mkuu wa polisi Gilbert Masengeli.