Mbunge wa Nyando Mheshimiwa Jared OKello alisema kuwa Cleophas Malala alikuwa anatafuta huruma kutoka kwa umma.
Alikuwa akizungumza katika mahojiano na runinga moja nchini mnamo tarehe 10 Aprili ,2025 ambapo alisema kuwa juhudi za aliyekuwa Seneta wa Kakamega Cleophas Malala alikuwa anajitafutia sifa kutoka kwa wananchi.
'' Ceophas Malala si mwandishi wa vitabu wala mwandishi wa mashairi kwa vyovyote vile kwa hivyo kusema kuwa alikuwa anapanga kuzindua kitabu cha tamthilia cha Echoes of War hiyo ilikuwa ni njia mojawapo ya kutaka kujipalia sifa na huruma kutoka kwa wananchi.
Malala kwanza alitaka kujinadi na kuonyesha umma kuwa alikuwa akitendewa unyama hata unapotazama katika video ambayo tuliona siku ya tarehe 9 Aprili , 2025 usiku saa tatu utajiuliza ni kwa nini alikuwa mahali pale wakati huo?
Tena aliweza kusababisha hali ya sintofahamu kwa kuweza kuwavutia watu wengi kuashiria kuwa alikuwa na nia fiche ya kuonyesha umma kuwa alikuwa akifanyiwa matendo mabaya ilihali si hivyo.
Hata unapotazama kulikuwepo na maafisa wa polisi ndio lakini aliweza kujinadi na kujitanua ili kuonyesha serikali kuwa ilikuwa katika upande mbaya wa kumshika bila makosa hata aliweza kusababisha baadhi ya wanahabari kutoka idhaa mbalimbali kama Maryann Nyambura waliokuwa wakitekeleza wajibu wao kisheria kupigwa na vitoza machozi hadi kuumia bure'' Okello alisema.
Kwa upande mwingine Malala alikuwa pale kaunti ya Nakuru ambapo michezo ya Drama kiwango cha kitaifa iliuwa yafaa kuigizwa.
''Mbona mnataka kunishika je, nimetekeleza kosa lipi?Mbona mnishike bila makosa yoyote?''
Malala aliuliza maswali mengi kwa mkuu wa kiengo cha DCI eneo la Nakuru alikuwa na msururu wa maswali mengi huku kando yao kulingana na video iliyowanasa kukiwa na maafisa wengi wa polisi wakiwa wamesimama kando yao.
Malala alikuwa ameandika Tamthilia kwa jina Echoes of war tamthilia ambayo ilikusudiwa kuigizwa na wanafunzi wa shule ya upili ya wasichana ya Butere.
Kulingana na duru za kuaminika ni kuwa tamthilia hiyo ilikuwa na maudhui ambayo yalikuwa yanalenga kuikosoa na kuchambua masuala mengi ambayo yalikuwa yamejikita katika mambo ya uongozi na utawala.
Kutokana na hilo serikali iliazimia kusimamisha uigizaji wa drama hiyo na vilevile kuwazuia wanahabari kuweza kunasa picha na video za wanafunzi hao wakiigiza.
Inasemekana kuwa uongozi wa shule hiyo kupitia kwa mwalimu mkuu uliazimia kufutilia mbali uigizaji wa tamthilia hiyo kutokana na hali tete ambayo imeibuka na vita vya kimasilahi kati ya serikali na shule hiyo.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!