
Waziri wa afya Aden Duale allihudhuria shughuli ya kutiwa sahihi kwa mkataba wa utendakazi wa fedha wa mwaka 2024/2025.
Mikataba hiyo ya utendakazi ilifanyika na mashirika ya kiserikali ya Semi Autonomous government na bodi za udhibiti katika izara ya afya.
Katika wizara hizo Duale alisisitiza umuhimu wa mikataba ya utendakazi katika idara za serikali akisema kuwa huweza kusaidia kuweka rekodi ambayo imenyooka ambayo huwa imelingana na hitaji la sera za kitaifa.
Alisema kuwa hiyo mikakati hueza kufanikisha uajibikaji na huhimiza mazoea ya kuweza kutekeleza nakudumisha matukio kwa wizara nzima katka idara na afisi za mawakala.
''Tupo katika wakati wa muhimu sana katika idara ya afya, Matarajio kutoka kwa mheshimiwa Rais na wananchi wa Kenya yako juu sana hasahasa katika mpango mzima wa kutekeleza bima ya matibabu ya SHI katika mfumo wa taifa care.'' Duale alisema haya akirai mashirika hayo kwa kusema kuwa ni lazima yajitahidi ili kupunguza makosa ya moja kwa moja.
Alisema kuwa mikataba ya mwaka huu ililenga kuhakikisha kuwa inaimarisha mpango wa SHI ambao kwa kufanya hivyo unatekelezwa pamoja na programu ambazo ni muhimu ili kufanikisha mpango maalumu wa huduma za afya kwa wote alimaarufu UHC.
Duale alizidi kusisitiza kwa kusema kuwa uhitaji wa mpango huo kwa kuimarisha viwango vya afya katika viwango vya kitaifa alieleza na kusisitiza kuhusu SAGA ili kuhakikisha kuwa wizara inaimarika zaidi na inaongeza utendakazi wake ili kupunguza visa vya ufisadi ndani ya wizara.
Utiaji sahihi wa mipango hio ilieza kuakisi mkataba mwingine ambao Rais alikuwa ameutia sahihi na mawaziri wa afya waliotangulia kwa ushirikiano na makatibu wa kudumu wa afya.
Lakini mpango huo uliweza kucheleweshwa kutokana na ukaguzi na udhibitishaji wa stakabadhi husika ingawaje aliweza kusema kuwa baadhi ya mashirika yalikua tayari yameanza utekelezaji huo kuashiria ile hali ya kujitolea kisawasaswa katika kufanikisha mpango huo.
Waziri aliweza kuwarai viongozi wa mashirika mbalimbali kuweza kujiwekea viwango vya utendakazi katika mashirika yao na akasisitiza kuwa wafanyakazi wataweza kupigwa msasa kutokana na matokeo ya rekodi ya utendakazi kwa kuangazia mambo kama heshima, maadili,ushirikiano na matumizi mazuri ya maliasili.
Duale alikua pamoja na katibu wa kudumu katika wizara ya afya Mary Muthoni, afisa wa afya katika hospitali za umma Harry Kimtai pamoja na mkurugenzi wa afya Daktari Patrick Amoth.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!